Tuesday, February 09, 2016

TANZANIA KUENDELEZA UTAFITI WA BIOTEKNOLOJIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Uvuvi, Dk. Florens Turuka (kulia), akizungumza na watafiti wa kilimo Dar es Salaam leo asubuhi, wakati akifungua mkutano wa nane wa mradi wa mahindi yanayostahimili ukame na kupambana na wadudu waharibifu wa Wema wa siku tatu wa watafiti kutoka nchi za Afrika wa kutathimini utendaji kazi wa Wema kwa mwaka uliopitaKushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kimataifa la Uharishaji wa Teknolojia za Kilimo (AATF), Dk. Denis Kyetere na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk.Hassan Mshinda.
Mkurugenzi wa Ushirikiano Mradi wa Wema, Kampuni ya Monsanto, Mark Edge (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
Ofisa Mkuu wa Programu, Taasisi ya Bill and Melinda Gates Dk.Lawrence Kent (kulia), akizungumza kwenye mkutano huo.
Meneja Mradi wa Wema, Shirika la Kimataifa la Uhaurishaji wa Teknolojia za Kilimo (AATF), Sylvester Oikeh akizungumza katika mkutano huo.
Mtafiti wa Mahindi, Shirika la Kimataifa la utafiti wa ngano na mahindi (CIMMYT), Yoseph Beyene akizungumza kwenye mkutano huo.
Meneja Mfumo na Uzalishaji wa Mbegu (AATF), Gospel Omanya akitoa mada katika mkutano huo.
Watafiti na washiriki wakiwa kwenye mkutano huo.
Watafiti na washiriki wakiwa kwenye mkutano huo

No comments: