Saturday, February 27, 2016

HAYA NDIYO YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

Baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kuwataka waandishi wote wa habari za kiuchunguzi pamoja na watafiti kuweka hadharani na kuueleza umma kile kilichotokea Zanzibar, Waandishi na watafiti mabalimbalai wamejitokeza na vielelezo vinavyoeleza jinsi uchaguzi huo ulivyoharibika

Vielelezo hivyo ni Nakala za fomu namba MUR. 12A za matokeo zilizotoka katika vituo vya kujumuisha kura ambazo zilikuwa zimejazwa kimakosa.
Hii ni fomu kutoka Kituo cha Skuli ya Mabaoni namba 23801, Jimbo la Chonga namba 2909 fomu hii siyo halali kutokana na kukosa mhuri wa tume ya uchaguzi Zanzibar. Msimamizi wa kituo ni Khamis mkungwa Zaid.

Fomu nyingine inatoka katika kituo cha Urusi chenye namba 26503, katika jimbo la Jang’ombe namba 1940

A. Hii ni fomu kutoka kituo cha Gamba namba 2008
Hii ni fomu kutoka kituo cha Gamba namba 2008, Jimbo la Mkwajuni namba 1926, fomu hii imepoteza uhalali kwasababu imefutwafutwa na haina mhuri wala jina la msimamizi wa kituo.

B. Kituo cha Skuli ya Mwembe Makumbi
Hii ni fomu kutoka katika kituo cha Skuli ya Mwembe Makumbi namba 21618, Katika jimbo la Chumbuni namba 1931, fomu hii imekosa uhalali kwasababu imefutwa majina ya mawakala na kupandikizwa majina mengine juu ya maandishi ya kivuli.

C. Jimbo la Chumbuni namba 1937
Hizi mbili, fomu kutoka kiwanja cha mpira Masumbani namba 29304 kutoka jimbo la Chumbuni namba 1937, fomu hii inakosa uhalali kwa sababu haina mhuri , maandishi ya meandikwa tena kwa kalamu juu ya maandishi ya kivuli na saini imewekwa zaidi uya mara moja. Fomu ya pili ni kutoka jimbo la Chakechake jina la kituo na namba haisomeki, fomu hii inakosa uhalali kwasababu inamhuri ambao siyo wa Tume ya uchaguzi anzibar ni mhuri wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar ambao haupaswa kutumika katika fomu hii.

D. Mihuri ya kughushi
Fomu ya pili ni kutoka jimbo la Chakechake jina la kituo na namba haisomeki, fomu hii inakosa uhalali kwasababu ina mhuri ambao siyo wa Tume ya uchaguzi anzibar ni mhuri wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar ambao haupaswa kutumika katika fomu hii.

Matumizi ya Mihuri Bandia katika karatasi za kujumuishia matokeo ya wagombea nafasi ya Rasi wa Zanzibar.

E. Fomu zimejirudia zaidi ya mara moja
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa ZEC alisema utata wa matokeo ulianza pale wajumbe waliopelekwa Pemba kurudi na kuiarifu Tume dhidi ya matendo yaliyofanywa na wasimamizi wa ZEC Pemba hata hivyo wakati uchunguzi na mabishano yakiendelea Mmoja wa wagombea akaitisha wanahabari na kujitangaza ameshinda kwa matokeo ambayo kila mmoja wetu alishangaa sana,

Ni kitendo cha aibu na Fedheha kubwa wanaoshabikia hawakuona madhara yake,sijui alitoa wapi Takwimu ambazo zilitoa ushindi kwa wagombea wawili tu,tena ukijumlisha asilimia ni 100 inasikitisha sana,Shinikizo la kunitaka nimtangaze mshindi kinyume na taratibu lilinifanya niubebe msalaba kusimamisha na kufuta matokeo baada tu ya kuitisha fomu chache za uthibitisho mwandishi haya ndio tuliyakuta,Ni nusu ya uchaguzi wote kila jimbo ulichezewa

Tumejiridhisha watu wetu watendaji wa ZEC walio apa walifanya haya,kutumia mihuri ya Bandia kujaza hizi fomu kinyume na taratibu kama mnavyo ona alisisitiza Mzee Jecha kwa masikitiko akiwaonyesha waanndishi waliofika kuhoji nini kilitokea hasa.BLOG http://zanzibariamani.blogspot.com/

No comments: