Saturday, February 20, 2016

Museveni Ashinda Urais Uganda

Tume ya Uchaguzi nchini Uganda imemtangaza Rais Yoweri Museveni kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi.

Rais Museveni alipata kura 5,617,503 sawa na asilimia 60.75 ya kura zilizohesabiwa kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume hiyo Dkt Badru Kiggundu.
Mpinzani wake mkuu Dkt Kizza Besigye alipata kura 3,270,290 ambazo ni sawa na asilimia 35.37%.
Awali, waangilizi kutoka Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Madola walikuwa wamekosoa uchaguzi huo wakisema kulikuwa na kasoro nyingi.
Aidha walishutumu kukamatwa kwa mgombea wa upinzani Dkt Besigye na kuzimwa kwa mitandao ya kijamii.

No comments:

πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΊπŸ‡¬ DIPLOMASIA NA USHIRIKIANO WA TANZANIA–UGANDA WAZIDI KUIMARIKA

Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, amewasili katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo, tarehe 06 Agosti 2026, ...