Saturday, November 01, 2014

NHC watathmini utekelezaji wa ujenzi wa miradi



Meneja wa NHC Mkoa wa Tabora, Erasto Chilambo akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Isikizya zilizopo wilayani Uyui mkoani Tabora kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.

Meneja wa NHC Mkoa wa Dodoma, Itandula Gambalagi akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo, Kongwa Dodoma kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.

 Washiriki wa Semina hiyo Wenceslaus Tillya, Meneja wa NHC mkoa wa Temeke, Nehemia Msigwa, Meneja wa NHC Katavi na Daniel Nkya wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche juu ya mapitio ya Mpango Mkakati wa Shirika unaomalizika mwakani, ili kuuboresha kwa kipindi kijacho. Somo hilo lilitolewa kabla ya mawasilisho ya mameneja wa mikoa.
Meneja Mshauri Taasisi inayojishughulisha na mambo ya uchumi ya Deloitte Bw.Frederick Nsemwa, Mkurugenzi wa Watushi Housing Limited, Dk Fred Nsemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu wakifuatilia somo hilo
Wataalamu washauri wa semina hiyo  wakiwa pamoja na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu, James Rhombo na Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki Benedict Kilimba wakifuatilia semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Susan Omari akifuatilia kwa kina soma hilo la Delloite Touche.

Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fatuma Chillo akisisitiza jambo katika semina hiyo huku Mkurugenzi wa Fedha, Felix Maagi na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara, David Shambwe wakifuatilia.
Julius Ntoga wa Shirika la Nyumba la Taifa, William Genya, Joseph Mwanasenga, Ramadhani Macha, Elias Msese, Pauline Mrango , Hamad Abdallah na Ladislaus Bamanyisa wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akisisitiza jambo katika semina hiyo.
Humphrey Kishimbo, Meneja wa NHC, Iringa, George Magembe, Meneja Miradi wa NHC na Mektilda Mihayo, Meneja wa Mahusiano kwa Wateja wakifuatilia somo katika semina hiyo.



 Washiriki wakifuatilia mada iliyotolewa na Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.

 Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.wakiwa na mdau kutoka Hydraform Tanzania wakifuatilia semina hiyo

No comments: