Tuesday, November 11, 2014

MAREHEMU HAMIS KIUMBU AMIGOLAS AZIKWA MAKABURI YA KISUTU

0Mwili wa Marehemu Hamis Kayumbu Amigolas  akiwekwa kwenye gari mara baada ya kutolewa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya taifa ya Muhimbili jana tayari kwa mazishi ambayo yalifanyika jana arlasiri kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam ambapo wanamuziki , ndugu  jamaa na marafiki mbalimbali pamoja na waombolezaji wengine walijitokeza kwa ajili ya kumzika marehemu Amigolas ambaye aliwahi kutamba na bendi ya African Stars Twanga Peteta kabla ya kweda Ruvu Stars Band ya JKT. 1Waumini wa Dini ya Kiislamu,  wakiusalia mwli wa aliyekuwa  mwanamuziki wa Ruvu Stars Band na Twamga Pepeta huko Mburahati Kinondoni jijini Dar es salaam kabla ya kwenda kumzika.2Waombolezaji wakiubeba mwili wa marehemu Hamis Kiumbu Amigolas5Wasani mbalimbali wakijadiliana jambo  katika makaburi ya Kisutu baada ya kuuhifadhi mwili wa marehemu Hamis Kiumbu Amigolas.6Waombolezaji wakisawazisha kaburi la  aliyekuwa mwana muziki wa Twanga Pepeta  katika makaburi ya Kisutu Baadhi ya  Waombolezaji wakiwa  wanauweka mwili wa marehemu Hamis  Kayumbu ‘Amigolas’,  Aliyekuwa  Mwanamuziki wa bendi ya Ruvu Stars Band  na African Stars  Twanga Pepeta  Dar es Salaam jana katika Makaburi ya  Kisutu.(PICHA NA KHAMISI MUSSA)

Mwili wa marehemu, Khamis Kayumbu ‘Amigolas’ ukibebwa na waombolezaji kuelekea katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.Msanii wa Filamu nchini, Jacob Steven 'JB' (wa pili kutoka kulia) akielekea makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.Waombolezaji wengine wakijiandaa kuelekea katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.Viongozi wa dini ya Kiisilam wakiomba dua mara baada ya kuzika marehemu Khamis Kayumbu ‘Amigolas’ kwenye makaburi ya Kisutu Jijini Dar jioni ya jana.Hili ndilo kaburi alimozikwa Marehemu Khamis Kayumbu ‘Amigolas’.

MAZIKO ya mwanamuziki wa zamani wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Khamis Kayumbu ‘Amigolas’ aliyefariki juzi amezikwa jana katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kuhudhuria na mamia ya watu.

No comments: