Friday, November 07, 2014

SHULE YA MSINGI KAWANZIGE ILIYOKO HALMASHAURI YA MJI WA MPANDA YAENDELEA KUFANYA VIZURI

unnamed1
Mwanafunzi wa shule ya msingi Kawanzige wakicheza baada ya kutoka madarasani wakijiburudisha kwa michezo wakati wa mapumziko hapo shuleni.
……………………………………………………………………………
Na Kibada Kibada -Katavi.
Pamoja na Changamoto lukuki zinazoikabili Shule ya Msingi Kawanzige iliyoko Halmashauri ya Mji wa Mpanda  Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi nje kidogo ya Mji umbali wa takribani kilometa 30 kutoka  mjini bado shule hiyo imeonekana kufanya vizuri katika matokeo ya elimu ya Msingi kwa mwaka  yalitangazwa na Baraza la mitihani la taifana  kushika nafasi ya kwanza kwenye shule zilizoko kwenye  Halamshauri hiyo.
Shule hiyo ambayo imeshika nafasi ya kwanza kwa Halmashauri ya mji na kuzigalaghaza shule zilizoko mjini ambazo zinapata kila aina ya  mahitaji yote muhimu.
Shule ya Kawanzige yenye idadi ya walimu kumi  kati yao saba wa kiume na watatu wa kike ina Idadi ya wanafunzi Wanafunzi 484 kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, ambapo wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba walikuwa wanafunzi 23 kati yao wanafunzi wa kiume walikuwa  na wakike
Shule hiyo ilishika nafasi ya kwanza katika halamshauri hiyo yenye shule 24 na nafasi ya pili kimkoa kati ya shule 159 nafasi ya 430 kitaifa kati ya shule 15867 za msingi nchi hivyo kuwa na wastani wa 174,0000.
Matokeo hayo yanaifanya shule kuwa moja ya shule bora pamoja na kuwa katika mazingira magumu kwa kutokuwa na vyumba vya madarasa wanafunzi madarasa tofauti kusomea kwenye chuma kimoja kwa wakati mmoja darasa la tatu na la tano, na wale wa darasa la kwanza na pili nao kuwa katika darsa moja huku wakiwa hawana madawati wakika chini changamoto ambayo inahitaji kupatiwa ufumbuzi.
Mbali ya changamoto hiyo kwa wanafunzi vitabu vya kiada na ziada ni shida maji hakuna matundu ya vyo ni shida,na walimu nao wanakabiliwa na changamoto lukuki kama ukosefu wa makazi bora, nyumba za kuishi hakuna,motisha kidogo kutoka kwa wakuu wao wa kazi hali iliyopelekea kutoa malalamiko yao kwa mkuu wa wilaya aliyetembelea shule hiyo kujionea changamoto zinazowakabili na kuwatia moyo waskate tama wawe na moyo wa kulipenda Taifa lao wakati Serikali inaendelea kushughulikia madai yao.
Pamoja na changamoto hizo bado walimu hao hawajakataa tama waliendelea kuchapa kazi kwa ushirikiano mkubwa na moyo wa kuipenda nchi yao pamoja na kuelewa changamoto zilizoko mbele yao hali iliyochangia kfanikisha ufaulu huo na kufanya vizuri huku wakiziacha mbali shule nyingine ambazo zinapata mahitaji muhimu na zina pata mahitaji muhimu ya huduma za kielimu na pia watoto wanasoma masomo ya ziada kwa kuwa hata umeme upuo.
Kutokana na hilo mkuu wa wilaya ya M,panda Paza Mwamlima amemwagiza mkurugenzi kupitia Idara ya Elimu Halmashauri ya mji kuona namna ya kuweza kuzipatia changamoto ufumbuzi na kuhakikisha madai na stahili za walimu wanatimiziwa ili waendelee kuchapa kazi na kulijenga taifa kwa kuelemisha watoto ambao watakuja kuwa viongozi wa baadaye wa Taifa hili.

No comments: