Thursday, November 20, 2014

KINANA ASHIRIKI KILIMO KATIKA SHAMBA LA UFUTA LA KIKUNDI CHA (UMOJA RIKA) KATIKA KIJIJI CHA MKOTOKUYANA NACHINGWEA

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh.  Mathias Chikawe wakati alipowasili katika kijiji cha Mkotokuyana jimbo la Nachingwea katika mwendelezo wa ziara yake ya mikoa ya Lindi na Mtwara itakayomchukua siku 16 akikagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa  na srikali kwa pamoja na wananchi huku akihimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi katika vijiji mbalimbali , Majimbo na wilaya Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-NACHINGWEA-LINDI)3Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akizungumza na  Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe. Regina Chonjo mara baada ya msafara wa Katibu Mkuu kuwasili katika kijiji cha Mkotokuyana4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliiza Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe. Regina Chonjo mara baada ya kufika kwenye shamba la ufuta la Kikundi cha Umoja Rika  jana kijijini hapo, Kulia ni Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe na kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi5Baadhi ya akina mama wanakikundi hichi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM huku wakiwa wameshika majembe yao.6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na Mbunge wa jimbo la Nachingwea wakikagua shamba la Mkotokuyana 7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kilimo katika shamba hilo huku  Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe akiwa amepanda akishuhudia kazi hiyo.8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akiendelea na kazi9Pamoja na vumbi kubwa kutimka wakati akifanya kazi hiyo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliendelea na kazi.10Kilimo kimepamba moto16Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Naipanga Nachingwea.15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi katika kijiji cha Naipanga14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jiko la shule ya Sekondari Nachingwea High School.12Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mh. Mathias Chikawe akishiriki katika kusafisha shamba la ufuta katika kijiji cha Mkotokuyana.11Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kung’oa visiki katika shamba la wananchi la kijiji cha Mkotokuyana wilayani Nachingwea jana.

No comments: