Friday, November 07, 2014

SKYLIGHT BAND YAZIDI KUWABAMBA MASHABIKI WAKE WA MUZIKI WA LIVE, TUKUTANE BAADAE THAI VILLAGE

DSC_0225Majembe ya Skylight Band yakitoa burudani ya kukata na shoka kwa mashabiki wao Ijumaa iliyopita ndani ya ukumbi wa Thai Village Masaki jijini Dar..Kutoka kushoto ni Aneth Kushaba AK47, Mkongwe wa muziki wa dansi Joniko Flower, Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa bongo, Digna Mbepera na Sam Mapenzi.
DSC_0179Sehemu ya umati wa mashabiki wa Skylight Band wakiburudika na sebene la Nasaka Dough ndani ya kiota cha Thai Village Masaki Ijumaa iliyopita.
DSC_0242Kikosi kazi cha Skylight Band kikiongozwa na rapa Joniko Flower kutoa burudani kwa mashabiki wake (hawapo pichani) Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha maraha cha Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0244Kutoka kushoto ni Aneth Kushaba AK47, Sony Masamba, Bela Kombo, Sam Mapenzi na Digna Mbepera wakijibu mapigo ya mashabiki wa Skylight Band kwa staili ya aina yake.
DSC_0254Mashabiki wa Skylight Band wakijibu mapigo kwa staili ya “Yachuma chuma”…Muguu wa kushoto mbele wa kulia nyuma, Yachuma chuma nataka mukanda Yachuma chuma….raha iliyoje unakosaje sasa, fanya uje tukutane pale kati.
DSC_0255Na huku nako hawavumi lakini wamo kama inavyoonekana pichani.
DSC_0261Wadau nao wakaendelea kujiachia……Asanteni kwa kuja na kuitakia wito wa Ukodak kwa sana bila woga…!
DSC_0013Divas wa Skylight Band wakiongozwa na Meneja wa bendi Aneth Kushaba AK47 kutoa burudani kwa mashabiki wao. Kulia ni Bela Kombo na kushoto ni Digna Mbepera kwenye show iliyowabamba wakazi wa jiji la Dar Ijumaa iliyopita ndani ya Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0174Wadada warembo kama hawa wanapatikana Skylight Band pekeee…ni Kila Ijumaa ndani ya Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0017Digna Mbepera akifanya yake huku akipewa back up na Aneth Kushaba AK47.

No comments: