Friday, November 21, 2014

SKYLIGHT BAND YAENDELEA KULAMBA DUME KWA MASHABIKI WAKE JIJINI DAR NDANI YA KIOTA CHA THAI VILLAGE

DSC_0016
Majembe ya Skylight Band yakiporomosha burudani kwa mashabiki wake Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar. Kutoka kushoto ni mkongwe kwenye muziki wa dansi Joniko Flower a.k.a Baba lao, Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa Bongo na Sam Mapenzi.
DSC_0087
Pichani juu na chini ni mashabiki nao wakijibu mapigo ya sebene lililokuwa likiporomoshwa na majembe ya Skylight Band.
DSC_0089
DSC_0020
Kutoka kushoto ni mkongwe kwenye muziki wa dansi Joniko Flower a.k.a Baba lao, Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa Bongo na Sam Mapenzi wakiwapa raha mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0121
Usishangae kumuona Sony Masamba kavua shati na kubaki na vest..ilikuwa ni patashika na nguo kuchanika…Joniko Flower akisongesha burudani.
DSC_0033
SAM MAPENZI…..Kuna watu hatari, wenye mapenzi zenye siri kali…Letu nalo lina jua kali, penzi letu serikali…Wajua nakupenda, malaika…….ANETH KUSHABA AK47:……Kuna wengi walafi, fimbo zao haziui mbali…Wengi wao wajidai, mimi kwako no, sitawai…Mmm take me, nitembee nawe….Baby take me, nitembee nawe… bonge moja la kolabo njoo ulishuhudie mwenyewe kwa macho yako.
DSC_0030
DSC_0059
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akifanya yake jukwaani kuhakikisha mashabiki wake wanapata furaha na tabasamu nyusoni mwao, usikose usiku wa leo ndani ya Thai Village kuanzia saa tatu usiku.
DSC_0085
Mashabiki wa Skylight Band wakijinoma na muziki mzuri kwa kujinafasi ndani ya kiota cha Thai Village Ijumaa iliyopita.
DSC_0021
If I should stay…..I would only be in your way…..So I’ll go but I know…I’ll think of you every step of the way…..And I… will always love you, ooh….Will always love you…You….My darling, you…….Mmm-mm…si mwingine ni Bela Kombo katika hisia kali za kuteka mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita ndani ya Thai Village, tukutane baadae kwa play list kali na nyimbo kali zilizoenda shule.
DSC_0043
Bela Kombo akiimba na zawadi ya ua kutoka kwa shabiki aliyekunwa na wimbo huo.
DSC_0115
Hashim Donode akifanya yake huku akipewa sapoti na mwanadada Bela Kombo.
DSC_0108
Rappa Joniko Flower akiporomosha mistari huku waimbaji wenzake wakisebeneka jukwaani.
DSC_0093
DSC_0133
Mashabiki nao walicharukaje sasa…..palikuwa hapatoshi uwanjani.

No comments: