Thursday, November 06, 2014

BALOZI WA RWANDA NCHINI AKUTANA NA KINANA

Balozi wa Rwanda nchini Eugene S. Kayihura akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za CCM Makao Makuu Ofisi Ndogo Lumumba jijini Dar es salaam.
Balozi wa Rwanda nchini Eugene S. Kayihura akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi za CCM Ofisi Ndogo Lumumba ambapo alikuwa na maongezi na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Eugene S. Kayihura .Balozi wa Rwanda nchini Tanzania amekutana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye Ofisi Ndogo za CCM Lumumba akiongozana na Msaidizi wa Balozi Ndugu Ernest Bugingo.

No comments:

DKT. ABBASI AKAGUA MIRADI YA UTALII PORI LA AKIBA LA PANDE, ATOA MAAGIZO YA KUKAMILIKA KABLA YA AFCON 2027

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, leo Julai 23, 2026, ametembelea Pori la Akiba la Pande jijini Dar es Salaa...