Monday, February 03, 2014

Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Kikwete Kwenye Shamrashamra za kilele cha maadhimisho ya sherere za miaka 37 ya CCM

Shamra shamra za kilele cha maadhimisho ya sherere za miaka 37 ya CCM,iliyofanyika ndani ya uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine,jijini Mbeya leo.PICHA NA IKULU

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwapungia wananchi  alipowasili kwenye maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa chama hicho kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya leo. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. JK aliimpongeza Kinana kwa kuonesha  njia na kutoa mfano kuhusu kufanya kazi ya chama ndani ya umma. Katika ziara zake mikoani akifduatana na baadhi ya makatibu wa Sekretarieti na viongozi wengine wa CCM, amekuwa  anafanya kazikubwa na nzuri sana . Na kwamba ziara zake zinakijenga chama na kutoa tawsira nzuri ya chama katika jamii. Pia alisema ziara za Kinana zinahuisha uhai wa chama.

Ndugu Kinana amekuwa anafanya  mambo  ambayo hayajazoeleka kufanywa. ametembelea maeneoa ambayo si viongozi wengi hufika. Wakati mwingine amekuwa anatumia njia za usafiri zinazoogopesha wengi. Hukaka na wananchi, anakula nao na kufanya nao kazi. Na kubwa zaidi amekuwa anatoa fursa kwa wananchi kuelezea matatizo yanayowasibu, manung'uniko yao na kero zao.. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Kinana akihutubia wakati wa maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa chama hicho, ambapo alisisitiza kuendeleza utaratibu alionao wa chama hicho kuwa karibu na wananchi, pamoja na kuisimamia Serikali katika utekelezaji wa Ilani ya chama hicho.
 JK akionesha mfano wa Jembe na Nyundo alama za chama hicho zinazomaanisha kwamba nchi inaongozwa na wafanyakazi na wakulima.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii maarufu nchini, baada ya kuwakabidhi kadi za kujiunga na chama hicho, wakati wa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, jijini Mbeya
 Kinana akiwapiga picha wamiliki wa mitandao ya kijamii (Bloggers) waliokuwa wakipiga picha ya paoja na Rasi Kikwete baada ya maadhimisho kumalizika.
 Wafuasi wa CCM waliotimiza miaka 37, wakirusha njiwa 37 ikiwa ni ishara ya kuadhimisha miaka 37 ya kuzaliwa kwa chama hicho.
 Msanii Ummy Wenslaus (Dokii), akionesha vimbwanga vyake alipokuwa akitumbuiza kwa wimbo wake wa CCM wakati wa sherehe za maadhimisho hayo.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kushoto) na  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Rungwe,  Richard Kasesera (kulia) wakicheza ngoma ya ling'oma wakati wa maadhimisho hayo.
 Kundi la TOT likiongozwa na Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa likifanya mambo wakati wa maadhimisho hayo
 Wasanii wa muziki na filamu wakiwapungia mikono wananchi baada ya kujiunga na CCM leo
 Seehemu ya umati wa wananchi ukiwa katika sherehe za maadhimisho hayo
 JK akimkabidhi nyaraka mlemavu wa mikono ambayo alimwahidi akiwa ziarani Mbeya siku zilizopita
 JK akitimiza ahadi kwa kumkabidhi Bajaji mlaemavu wa miguu
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete (katikati) akipiga gita alililinunua kwa ajili ya kumpatia msaada msanii (kuia) wa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii maarufu nchini, baada ya kuwakabidhi kadi za kujiunga na chama hicho, wakati wa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, jijini Mbeya
 JK akikabidhi gitaa hilo, iiwa ni kutimiza ahadi aliyomwahidi msanii huyo mwaka jana
 Msanii huyo akiwa na furaha baada ya kukabidhiwa gitaa hilo
JK  na Kinana wakiwa katika picha ya pamoja na vijana wa vyuo vikuu waliojiunga na chama hicho

No comments: