Thursday, February 27, 2014

UZINDUZI RASMI WA KAMPENI YA TAIFA YA KUSAMBAZA UELEWA WA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA WANANCHI WAFANYIKA

Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu  akizindua rasmi vipeperushi vilivyo andikwa , Mambo Saba makubwa ya kuungwa mkono na wananchi katika Rasimu ya Katiba pamoja na mambo makubwa matano yanayokosekana katika Rasimu ya Katiba na Kipeperushi cha pili kinacho sema ‘Taifa ni letu na Katiba ni yetu Husika tupate Katiba Bora.
 Jaji Mkuu Mstaafu Mh. Thomas Mihayo akitoa ufafanuzi wa uzinduzi wa Rasimu ya pili ya Katiba
 Mkurugenzi Mtendaji wa Haki za Binadamu Bi. Helen Simba akieleza kuhusika kwa haki za Binadamu katika Rasimu ya Pili katiba kwa wananchi.
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akitoa hotuba kabla ya uzinduzi Rasmi wa kampeni ya Taifa ya kusambaza uelewa wa Rasimu ya Pili ya Katiba kwa Wananchi
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu  akizindua Rasmi Kijitabu kidogo kilicho andikwa Rasimu ya Pili ya Katiba Inasemaje? Chapisho la Lugha nyepesi
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akigawa vipeperushi hivyo kwa ishara ya uzinduzi rasmi.
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akizindua Rasmi Jarida la Rasimu ya Pili ya Katiba 
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akizindua Flash Disk maalum zenye Rasimu ya Katiba ambazo zitagawiwa kwa waendesha Bodaboda ili abiria akipanda nae apate kusikiliza Rasimu hiyo.
Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akizindua Rasmi, DVD, VCD pamoja na AUDIO CD kwa ajili ya walemavu.
Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu akizindua Rasmi Tovuti ‘Blog’ inayo itwa Taifa ni letu www.taifaniletu.blogspot.com ambayo ni maalumu kwa ajili ya Rasimu ya Pili ya Katiba.
 
 Mgeni Rasmi Makamu Mwenyekiti Tume za haki za Binadamu Bi. Maafudha Hamidu  akitoa pongezi kwa jinsi mchakato unavyokwenda ikiwa ni pamoja na kutumia Teknolojia ya hali ya juu ili kila mtu afikiwe na Rasimu ya Pili ya Katiba
 Kundi la watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali wakiwa wamefika katika uzinduzi wa kampeni ya taifa ya kusambaza uelewa wa Rasimu ya Pili ya Katiba kwa wananchi wote
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jangwani wakiwa katika uzinduzi wa kampeni ya taifa ya kusambaza uelewa wa Rasimu ya Pili ya Katiba kwa wananchi wote,ambapo pia kulikuwa na shule zengine Kama Azania ,Mazimbwi na Chamazi.
Picha na Dar es salaam Yetu Blog

No comments: