Wednesday, February 05, 2014

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

KUHAMA KWA OFISI ZA   MAKAO

 MAKUU YA SHIRIKA




Tunapenda kuwafahamisha wateja wetu na umma  kwa ujumla kuwa Ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa zimehamia kwenye jengo lake  jipya lililopo Kiwanja Na. 1   kwenye makutano yaBarabara za Ufukoni na Ally Hassan Mwinyi,  eneo la Upanga Jijini Dar es salaam.
Aidha, tunapenda kuwaomba wateja wetu wa Dar es Salaam kwamba wakati Shirika likiendelea kukamilisha zoezi la kuhamisha ofisi zake waendelee kupata huduma katika ofisi za Mikoa ya Shirika za Ilala, Temeke, Kinondoni na Upanga.
Utaratibu wa kuhamisha Makao Makuu ya Shirika  unafuatia maboresho mbalimbali yanayofanywa na Shirika tangu mwaka 2010 kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa miaka mitano 2010/15 unaolenga kuboresha huduma kwa wateja na wananchi kwa ujumla.


IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA


No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...