Monday, February 17, 2014

Frank Sanga ameteuliwa kuwa Mhariri Mtendaji Mpya wa Gazeti la Mwananchi

 Frank Sanga 
--
 Idara ya Habari ya Mwananchi Communications Ltd, imetangaza mabadiliko ya Uongozi kutokana na kuondoka kwa baadhi ya waliokuwa wahariri wa gazeti hilo.
 
Katika mabadiliko hayo Frank Sanga ameteuliwa kuwa Mhariri Mtendaji mpya wa Gazeti la Mwananchi akichukua nafasi iliyoachwa na Dennis Msacky. Kabla ya uteuzi huo, Sanga alikuwa Mhariri Mtendaji wa Mwanaspoti, nafasi ambayo imezibwa na Abdul Mohamed.
 
Uteuzi mwingine ni wa Reginald Miruko ambaye anakuwa Mhariri wa Habari (News Editor) wa Mwananchi, akichukua nafasi ya Samson Mfalila ambaye ali-resign mwishoni mwa wiki iliyopita.
 
Neville C. Meena,
Cell: +255 - 787 - 675555
        +255 - 753 - 555556

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...