Friday, February 28, 2014

Rais Kikwete azindua Rasmi Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa mawasiliano ya Simu


  Mgeni Rasmi Kuwasili Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho kiwete ,  Rais wa Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizindua Rasmi Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa mawasiliano ya Simu kwa kukata utepe ambapo sherehe hizo zilifanyika  Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya  Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) aliouzindua leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia niWaziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pro, Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ProfJohn Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama.

 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe  kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam.


 Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho kiwete ,  Rais wa Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa akiwa katika 'Laptop' kwa ajili ya kubofya ili kuruhusu Rasmi mtambo huo kuanza kufanya kazi.

 
 


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Profesa John Nkoma akitoa Maelezo ya kina kwa Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho kiwete ,  Rais wa Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jinsi Mtambo huo unavyofanya kazi


 Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho kiwete , Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  akizungumza Jambo wakati wa uzinduzi Rasmi  wa Mtambo huo.

No comments: