Friday, February 28, 2014

Tume ya Taifa ya uchaguzi imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE kama ifwatavyo:-

 Tume ya taifa ya uchaguzi imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE, mtakumbuka kuwa jimbo hilo limekuwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo bwana Said Bwanamdogo kufariki dunia tarehe 22 Januari 2014 kwenye hospitali ya MOI jijini Dar es salaam. 

Ratiba ya uchaguzi kwenye jimbo hilo iko kama ifuatavyo:-
 
1. Uteuzi wa wagombea  - Tarehe 12 Machi 2014
 
2, Kampeni na Uchaguzi - Tarehe 13 Machi 2014
 
3. Siku ya Uchaguzi - Tarehe 6 April, 2014
 


Tarehe ya wagombea ubunge kuchukua Fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi ni kuanzia tarehe 03 Machi, 2014 hadi tarehe 12 Machi, 2014(Siku ya uteuzi) Kabla ya saa 10:00 Alasiri.
 

Wagombea wanatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi siku ya uteuzi si zaisi ya saa 10:00 Alasiri.

No comments:

🔴🔴TABORA ZOO YAENDELEA KUNG'ARA KAMA KITOVU CHA ELIMU, BURUDANI NA UTALII WA NDANI

Na Mwandishi wetu, Tabora. Bustani ya Wanyamapori Tabora (Tabora Zoo) imeendelea kujipambanua kama kivutio muhimu cha elimu na burudani jiji...