Friday, February 28, 2014

Tume ya Taifa ya uchaguzi imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE kama ifwatavyo:-

 Tume ya taifa ya uchaguzi imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo la CHALINZE, mtakumbuka kuwa jimbo hilo limekuwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo bwana Said Bwanamdogo kufariki dunia tarehe 22 Januari 2014 kwenye hospitali ya MOI jijini Dar es salaam. 

Ratiba ya uchaguzi kwenye jimbo hilo iko kama ifuatavyo:-
 
1. Uteuzi wa wagombea  - Tarehe 12 Machi 2014
 
2, Kampeni na Uchaguzi - Tarehe 13 Machi 2014
 
3. Siku ya Uchaguzi - Tarehe 6 April, 2014
 


Tarehe ya wagombea ubunge kuchukua Fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi ni kuanzia tarehe 03 Machi, 2014 hadi tarehe 12 Machi, 2014(Siku ya uteuzi) Kabla ya saa 10:00 Alasiri.
 

Wagombea wanatakiwa kuwasilisha fomu za uteuzi kwa msimamizi wa uchaguzi siku ya uteuzi si zaisi ya saa 10:00 Alasiri.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...