Tuesday, April 19, 2016

ZANTEL YAKABIDHI COMPUTER 21 KWA VYUO VYA WALIMU ZANZIBAR.

Afisa Mtendaji wa Millcom Africa Bi Cynthia Gordon akimkabidhi Computer Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma, anayeshuhudia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Zantel Tanzania Benoit Janin, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Zanzibar  
Afisa Mtendaji wa Millcom Africa Bi Cynthia Gordon akimkabidhi Computer Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma, anayeshuhudia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Zantel Tanzania Benoit Janin, Afisa wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussa Baucha na kushoto Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bi Khadija Juma Bakari,hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Zanzibar  
Maofisa wa Zantel wakifuatilia hafla hiyo ya kukabidhi Computer Vyuo vya Walimu Zanzibar.
Maofisa wa Zantel wakifuatilia hafla hiyo ya kukabidhi Computer Vyuo vya Walimu Zanzibar.
Afisa wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussa Baucha akitowa maelezo wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi Computer Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa ajili ya matumizi ya Vyuo vya Ualimu Zanzibar.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Zantel Tanzania Benoit Janin akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi Computer kwa ajili ya Matumizi ya Vyuo vya Ualimu Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Hyatt Shangani Zanzibar. Na kusema lengo la Zantel ni kushirikiana na Serikali kwa lengo la kukuza na kuboresha elimu ya teknolojia na mawasiliano kusaidia vyuo vya Ualimu vinavyotoa Mafunzo hayoili kuongeza ufanisi
katika ufundidishaji wao..
Afisa Mtendaji wa Millcom Africa, Bi Cynthia Gordon, akizungumza wakati wa hafla hiyo na kusema Walimu ndio msingi wa maendeleo kwenye Taifa na ndio maana Zantel imewapa kipaumbele katika miradi yake ya Kijamii. na Kusema Zantel Daima imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha tunaboresha sekta elimu kwa wazanzibari na kama tunavyojua elimu ya teknolojia na mawasiliano ni muhumu kwa dunia ya sasa. 

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Computer na Kampuni ya Simu ya Zantel kwa ajili ya Vyuo vya Ualimu Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa hotel ya Hyatt Shangani Zanzibar, na kuipongeza kampuni hiyo kwa jitihada zake inayofanya kwa kushirikiana na serikali katika kukuza na kuboresha elimu visiwani Zanzibar.
‘Ili kutoa elimu bora kwa walimu wa teknolojia ya mawasiliano wa ngazi zote ni muhimu kuhakikisha mafunzo ya komputa yanajumuishwa kwenye mtaala wa vyuo vya elimu ili kuwajengea uwezo walimu katika kufundisha wanafunzi’ 
Maofisa wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar wakifuatilia hafla hiyo ya makabidhiano ya Computer kwa ajili ya matumizi ya Vyuo vya Walimu Zanzibar.
Mkuu wa Vyo vya Ualimu Zanzibar Maulid Omar Hamad akitowa neno la shukrani kwa Uongozi wa Zantel Tanzania kwa msaada wao wa Computer 21 kwa ajili ya matumizi ya Vyo hivyo katika kutowa mafunzo kwa Walimu hao.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma Afisa wMtendaji Mkuu wa Zantel Benoit Janin.wakifuatilia hafla hiyo wakimsikiliza Mkuu wa Vyuo vya Walimu akitowa shukrani. 
Viongozi wa meza kuu wakimsikiliza Mkuu wa Vyuo vya Walimu Zanzibar Maulid Omar Hamad, akitowa shukrani kwa niaba ya Vyuo hivyo wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Computer na Kampuni ya Simu za Mkoni Zantel hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Zanzibar. 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma, Mtendaji Mkuu wa Zantel Tanzania Benoit Janin Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Zanzibar Bi Khadija Juma Bakari kushoto Afisa Mtendaji wa Millcom Bi Cynthia Gordon na Afisa wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussa Baucha wakiwa katika picha ya pamoja na Maofisa wa Zantel na Wizara ya Elimu Zanzibar.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amaali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma akibadilisha mawazo na Mtendaji Mkuu wa Zantel Benoit Janin na Mtendaji wa Millicom Bi. Cynthia Gordon, baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhi Computer kwa ajili ya Matumizi ya Vyuo vya Walimu Zanzibar.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma akitowa shukrani kwa Kampuni ya Zantel kwa msaada wao wa Computer kusaidia matumizi katika Vyuo vya Walimu Zanzibar. wakati akizungumza na waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Zanzibar.  
Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussa Baucha akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar baada ya hafla ya kukabidhi Computer 21 kwa ajili ya matumizi ya Vyuo vya Ualimu Zanzibar.
Imetayarishwa na othmanMapara.Blogspot.com.
Zanzinews.com.

No comments: