Tuesday, April 05, 2016

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA ARUSHA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utalii na Masoko Bw. Ibrahim Mussa (kulia) akiongea na Kaimu Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Arusha Bi. Maria Kirombo (kati) na Mhifadhi wa Idara ya Ulinzi Bw. Haima Hera muda mfupi kabla ya kuwasili kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa ziara fupi hifadhini hapo.
tana2Kaimu Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Arusha Bi. Maria Kirombo akitoa maelezo mafupi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kabla ya kuanza kwa ziara fupi katika Hifadhi ya Arusha.
tana3Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ndani ya basi dogo wakiangalia wanyama aina ya nyati wanaopatikana katika Hifadhi ya Arusha.
tana4Twiga watatu wakionesha mbwembwe zao mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.
tana6Waheshimiwa Joseph Kasheku ‘Msukuma’ (kulia) na Shaban Shekilindi (Lushoto) wakiwa na fuvu la mnyama nyati walilolikuta hifadhini hapo na kupiga nalo picha na kisha kuliacha hapo hapo.
tana7Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani (kushoto),Mhe. Joseph Kasheku ‘Msukuma’, Mhe. Kemilembe Julius na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Ibrahim Mussa katika picha ya pamoja.
tana9Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipowasili Hifadhi ya Taifa ya Arush
tana10Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani akiongea na watumishi wa Hifadhi ya Arusha mara baada ya kumalizika kwa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii

No comments: