Saturday, April 30, 2016

Ufunguzi wa Hypermarket kubwa kuliko Mwanza unaendelea hivi sasa katika Mall ya Rock City Mwanza.

Hypermarket hii ambayo ni tawi jingine jipya la TSN linatazamiwa kuwahudumia wakazi wa Mwanza waliokuwa wakikosa uhondo wa bidhaa mbalimbali kwa bei nafuu zikiwemo mbogamboga fresh kutoka hapa hapa nyumbani.

Akizungumza katika ufunguzi huo masaa machache yaliyopita Mkurugenzi wa TSN alisema,Tanzania Sisi Nyumbani  TSN itatoa zawadi kwa watu 100 wa mwanzo kufika katika uzinduzi huo. 

"Hii ni hatua nyingine kubwa ya kuhakikisha Watanzania wanapata vitu fresh.. kutoka nyumbani tena kwa bei nafuu.Tanzania Sisi Nyumbani tunahakikisha Watanzania wanafurahia mazao yao wenyewe...tena kwa bei ya gengeni katika Hypermarket hii.. Wateja wetu ni majirani zetu... karibuni sana TSN Hypermarket Mwanza." alisema.
 Sehemu ya mpnagilio wa bidhaa kwa ndani kama zinavyoonekana. 
 Sehemu ya malipo kwa ndani kama inavyoonekana
 Bidhaa ain ya mboga mboga fresh kabisa 
 Bidhaaa mbalimbali zikiwa ndani ya TSN,tayari kwa wateja kuanza 
Watu na wateja mbalimbali wamefika kujionea Hypermarket hiyo ya kisasa kabisa ndani ya jiji la Mwanza.

No comments: