Saturday, April 16, 2016

SERIKALI YA KOREA YAGHARAMIA UJENZI WA HOSPITAL YA CHANIKA UTAKAO GHARIMU BILIONI 8.8 ZA KITANZANIA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia) na Makamu wa Rais wa Shirika la Koica la nchini Korea Kusini, Taemyon Kwon, wakiweka tofali kwa pamoja kuashiria uweka wa jiwe la msingi la Hospitali ya Chanika iliyopo Manispaa ya Ilala, inayojengwa kwa ufadhili wa nchi hiyo Dar es Salaam jana. Ujenzi huo hadi kukamilika utagharimu sh. bilioni 8.8 za kitanzania.
.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Mr Isaya (kulia), Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala, Victriana Ludovic na Meneja wa Mradi wa ujenzi wa Hospitali hiyo Mr Kim wakiweka jiwe la msingi la Hospitali hiyo.
Meneja wa Mradi huo, Mr Kim akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na ujumbe wake ramani ya majengo ya Hospitali hiyo.Na Dotto Mwaibale
Hutuba na taarifa ya mradi huo zilisomwa.
Balozi wa Korea nchini Geum-young Song (katikati), akizungumza katika hafla hiyo.

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na balozi wa Korea nchini Geum-young Song wameweka jiwe la msingi la Hospitali ya Chanika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam ambapo itakapo kamilika itakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi 4000.

Akizungumza katika hafla ya kuweka jiwe hilo la msingi Chanika jijini Dar es Salaam jana, Makonda aliishukuru serikali ya Korea kwa msaada wa ujenzi wa Hospitali hiyo ambayo itawasaidia wananchi wa Chanika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Amana.

"Tunawashukuru hawa ndugu zetu wa Korea Kusini kwa msaada wa kutujengea Hospitali hii nawaombeni wananchi kuitunza ili kila mtakapokuwa mnafika kutibiwa tuwakumbuke wakorea" alisema Makonda.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala, Victorina Ludovic alisema ujenzi wa Hospitali hiyo utasaidia kusogeza huduma muhimu karibu na wananchi wapatao 398,882 kutoka maeneo ya Chanika, Msongola, Zingiziwa na Majohe hivyo kupunguza muda na gharama ambazo wananchi wamekuwa wakitumia kufuata huduma hizo umbali wa kilometa 30 kwenda hospitali ya Amana ya Rufaa.

Ludovic alisema ujenzi wa mradi huo hadi utakapokamilika utagharimu dola la milioni 4 sawa na sh.bilioni 8.8 za kitanzania.Balozi wa Korea nchini , Geum-young Song amesema wakorea hawafurahishwi wanapoona mama na mtoto wanapoteza maisha wakati wa kujifungua nchini Tanzania.

"Nchi yetu kupitia shirika la Koica imeamua kujitolea kujenga hospitali hii ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania kupata huduma bora ya afya ya mama na mtoto wakati wa kujifungua kwani hatupendi kuona wanapoteza maisha wakati wa kujifungua" alisema Young Song.

Balozi huyo aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na nchi ya Korea katika shughuli mbalimbali jambo linaloimarisha uhusiano baina ya wananchi wa nchi hizo.

No comments: