Sunday, April 10, 2016

BALOZI WA STARTIMES BARANI AFRIKA KANU AAHIDI MCHANGO WAKE KWA SOKA LA TANZANIA

KN1
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine (katikati) akimkabidhi jezi ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Balozi wa StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu kutoka nchini Nigeria, lengo ni kuthamini mchango wake.Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa  StarTimes Tanzania, Lanfang Liao.
KN2
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine, akizungumza na wadau wa mpira nchini kwenye hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kampuni ya StarTimes kwa lengo la kumkaribisha Balozi wa StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu kutoka nchini Nigeria.
KN3
Balozi wa StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu akizungumza na wadau wa mpira nchini kwenye hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kampuni ya StarTimes kwa lengo la kumkaribisha nchini mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine ameishukuru Kampuni ya StarTimes Tanzania kwa kuthamini soka kwa kumleta nchini mchezaji nguli wa kimataifa wa Nigeria, Nwanko Kanu.
Mwesiga aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam kwenye hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kampuni ya StarTimes kwa lengo la kumkaribisha Balozi wa StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu kutoka nchini Nigeria.
 “Kupitia StarTimes tutaboresha mpira wetu kwa kuangalia ligi mbalimbali za mataifa ya Ujerumani, Italia na Ufaransa” alisema Mwesigwa.
Ujio wa Kanu nchini ni fursa na unamanufaa makubwa kwa mustakabali wa ukuaji wa soka hasa kwa kuzingatia afya ya vijana katika michezo.
Kwa upande wake Balozi wa StarTimes barani Afrika Nwankwo Kanu ambaye alikuwa mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Nigeria (Super Eagles) amesema kuwa amekuja Tanzania kwa mwaliko wa StarTimes na kuahidi kurudi kwa shughuli zake za kimichezo maana amefurahishwa na mapokezi na anaamini mchango wake katika soka la Tanzania unahitajika.
“Mustakabali wa mpira wa miguu wa Tanzania utakuwa mkubwa kama Watanzania watapenda kufuatilia masuala ya mpira wa miguu kupitia ligi tofauti tofauti, kadiri unavyoangalia michezo mbalimbali ya kimataifa, ndivyo unavyozidi kujifunza” alisema Kanu.
Kanu alifanyiwa upasuaji wa moyo mwaka 1996 na ndipo alipoamua kufungua taasisi yake ya moyo inayoitwa “The Kanu Heart Foundation.”
Taasisi hiyo iliyoko nchini Nigeria ambako ndiko alipozaliwa aliianzisha kwa madhumuni makubwa ya kusaidia wagonjwa wenye matatizo ya moyo na ameahidi taasisi hiyo kushirikiana na taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika masuala mbalimbali ya kitabibu.
Kanu mbali na kuchezea timu yake ya Taifa, pia aliwahi kuchezea vilabu vya Iwuanyanwu Nationale kati ya mwaka 1992 hadi 1993, mwaka 1993 hadi 1996        alichezea AFC Ajax, mwaka 1996 hadi 1999 alichezea Inter Milan, mwaka 1999 hadi 2004 aliichezea Arsenal, mwaka 2004 hadi 2006 alichezea West Bromwich Albion na  mwkaa 2006 hadi 2012 alichezea Portsmouth. 

No comments: