Thursday, April 07, 2016

KAMPUNI YA MAFUTA YA TOTAL YAWAKABIDHI ZAWADI WASHINDI WA SHINDANO LA "START UPPER OF THE YEAR BY TOTAL CHALLENGE"

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki akizungumza katika hafla ya kuwakabidhi zawadi washindi wa shindano la wajasiliamali la kampuni ya Mafuta ya TOTAL iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya TOTAL Tanzania, Tarik Moufaddal akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa washindi wa shindano la wajasialiamali hapa nchini ambapo washindi watatu bora wajasiliamali walikabidhiwa zawadi zao na kampuni ya TOTAL katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Mradi wa Kampuni ya Mafuta ya TOTAL, Marsha Msuya akiwakaribisa wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya kuwakabidhi zawadi washindi wa shindano la wajasialiamali la Kampuni ya TOTAL katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa shindano la Kijasiliamali ya Kampuni ya TOTAL Tanzania wakiwa kwenye hafla hiyo kabla ya kukabidhiwa zawadi zao.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki(Kutoka kushoto wa pili) akiwa na viongozi wa Kampuni ya TOTAL Tanzania katika hafla ya kuwakabidhi zawadi washindi wa shindano la wajasiliamali la kampuni ya TOTAL hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

No comments: