Tuesday, April 19, 2016

MAHAFALI YA KIDATO CHA SITA YAFANA

Mgeni rasmi kwenye mahafali ya Kidato cha Sita kwa Shule ya Sekondari Tambaza ya Jijini Dar es Salaam, Injinia Haikamen Mlekio akivishwa skafu kukaribishwa kwenye mahafali hayo akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu kwenye jukumu la Huduma kwa Jamii.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Tambaza ya Jijini Dar es Salaam, Zuberi Hussein Mavumba akimkaribisha mgeni rasmi kwenye mahafali hayo yaliyofanyika leo.
Kikundi cha vijana wa Shule ya Sekondari Tambaza akitumbuiza kwenye hafla hiyo ya mahafali ya kidato cha sita.
Msanii Nick wa Pili ambaye alialikwa katika hafla hiyo kama role model akiwapa mkono wanafunzi wa kidato cha sita mara baada ya vijana hao kukabidhiwa vyeti na Mgeni Rasmi Injinia Haikamen Mlekio.
Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Injinia Haikamen Mlekio akikabidhi vyeti kwa vijana wa kidato cha sita waliofanya sherehe ya graduation yao leo.

 Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule hiyo leo.
 Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita waliofanya mahafali ya kuwaaga leo.

No comments: