Saturday, April 30, 2016

RC PAUL MAKONDA AZINDUA KAMPENI YA USAFI JIJI LA DAR LEO


Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh.Paul Makonda akiwahutubia Wananchi mbalimbali mapema leo asubuhi katika viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar mara baada ya kumaliza kufanya usafi na hatimae kukusanyika kwenye viwanja hivyo,ambapo Mh.Paul Makonda alizindua kampeni ya Usafi kwa jiji la Dar.

Mkuu wa Mkoa Mh.Paul Makonda akimkabidhi ufagio Mwenyeki wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Wilaya ya Temeke ndugu Bakari Makere,kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa Paul Makonda katika uzinduzi wa Kampeni hiyo ya Usafi kwa jiji hilo.

Mkuu wa Mkoa Mh.Paul Makonda akimkabidhi ufagio Mwenyeki wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Wilaya ya Kinondoni Ndugu Juma Mgendwa. 
Sehemu ya meza kuu ikifuatilia yaliokuwa yakijiri uwanjani hapo

No comments:

Compact Energies: Nishati ya Jua Ni Chachu ya Mageuzi ya Uchumi Tanzania

  Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Kitanzania ya Compact Energies, inayojihusisha na uzalishaji na usambazaji wa vifaa vya kisasa vinavyotumia n...