Wednesday, August 12, 2015

SIKU YA KIMATAIFA YA VIJANA YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.


 Bendi ya jeshi la polisi ikiongoza Maandamano ya siku ya vijana Duniani ,yaliyofanyika Agost 12 kila mwaka yaliyoanzia katika Shule ya Sekondari Jangwani na kuishia katika  viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
 Naibu Katibu  Mkuu wa Wizara ya habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo,Profesa Gabriel Ole Sante akizungumza  katika maadhimisho ya Siku ya Viajna Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.
 Vijana wakionyesha ujuzi wao katika mchezo wa sarakasi katika siku vijana duniani yaliyofanyika katika viwanja vya manzai mmoja leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Profesa Gabriel Ole Sante akipata maelekezo kutoka Afisa Maendeleo wa Vijana wa Wizara hiyo,Dora Meena katika maadhimisho ya Siku vijana Duniani yaliyofanyika leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo,Profesa Gabriel Ole Sante akipata maelezo katika banda la Asasi ya Vijana wa Umoja wa Matiafa (YUNA), katika maadhimisho ya Siku Vijana Duniani yaliyofanyika leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Vijana walioshiriki Maadhimisho ya Siku Vijana Duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)

No comments: