Monday, February 02, 2015

Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali wameishukuru Serikali kutoa elimu ya Ujasiriamali


Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Bibi Mariam A. Mtunguja (katikati) akizungumza na maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya kutembelea vijana wa Mkoa wa Mbeya na kutoa elimu ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Bw. Gullamhussein S. Kifu (katikati) wakati wa ziara ya kutoa mafunzo ya Ujasiriamali kwa vijana wa Wilaya hiyo. Kulia ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na anayefuata ni Kaimu Afisa Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bw. Athuman Mustafa Kinza.
Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele akiwaelekeza vijana wa Mbarali namna ya kuandika andiko la mradi wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyotolewa kwa vijana wa Mbarali hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Wood Works Bw. Stafford Gwimile (wa pili kulia) akizungumza na maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipotembelea mradi wa kikundi hicho kwa ajili ya kutathmini shughuli za vijana na utoa ushauri kwa vijana wa Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya.
Maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na vijana wa Kikundi cha Umati Sanaa Group wakiburudika na muziki uliokua ukitumbuizwa na vijana wa kikundi hicho wakati wa ziara ya kutembelea vikundi vya vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya.
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa (waliokaa kushoto) akizungumza na vijana wa Umati Sanaa Group wanaofanya kazi za sanaa walipofika kuangali kazi zinazofanywa na kikundi hicho wakati wa ziara ya uhamasishaji kwa vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya.(Picha zote na: Genofeva Matemu – Mbarali, Mbeya)

No comments:

SERIKALI YATOA ZAIDI YA BILIONI 5.7 KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA ELIMU MKOANI KIGOMA

KIGOMA: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP), imetoa zaidi ya Shilin...