Thursday, February 19, 2015

RAIS KIKWETE APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA MALAWI, KUWAIT AFRIKA YA KUSINI NA KENYA

1
Baliozi mpya wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Hawa Ndilowe akiwasilisha kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete hati za Utambulisho ikulu jijini Dar es Salaam Februari 18, 2015. Katikati anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Maharage Juma.
2
Balozi Ndilowe akiwa katika picha na Rais Kikwete na kufanya naye mazungumzo baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
3
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Baliozi mpya wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Hawa Ndilowemara mara baada ya kuwakilisha hati za Utambulisho.
4
Balozi mpya wa Kuwaiti nchini Tanzania Mhe.Jasem Ibrahim Al-Najem akiwasilisha kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete hati za utambulisho ikulu jijini Dar es Salaam Februari 18, 2015.
5
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania akiwa katika picha na Rais Dkt.Jakaya Kikwete.
6
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania na Rais Dkt.Jakaya Kikwete.wakiwa katika mazungumzo baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
7
Balozi Mpya wa Afrika ya Kusini nchini Tanzania Mhe.Thamsanqa Dennis Mseleku akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo. Katikati anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Maharage Juma.
8
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na balozi mpya wa Afrika ya Kusini nchini Tanzania Thamsanqa Dennis Mseleku baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho na kufanya naye mazungumzo.
910
Balozi Mpya wa Kenya nchini Tanzania Mhe.Chirau Ali Mwakwere akiwasilisha Kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete hati zake za utambulisho ikulu jijini Dar es Salaam leo. . Katikati anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Maharage Juma.
.1111
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania Chirau Ali Mwakwere wakikumbatiana na kwa furaha muda mfupi baada ya balozi huyo kuwasilisha hati zake za utambulisho ikulu jijini Dar es Salaam leo. (picha zote na Freddy Maro)

No comments: