Monday, February 23, 2015

YANGA YAICHAPA MBEYA CITY 3-1

MRISHO-NGASSA

VINARA wa Ligi Kuu Vodacom, Yanga, jana huko Sokoine, Jijini Mbeya wamepaa kileleni wakiwa Pointi 5 mbele ya Timu ya Pili na Mabingwa Watetezi, Azam FC, baada ya kuichapa Mbeya City Bao 3-1.
Bao za Yanga hii Leo zilifungwa na Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Amisi Tambwe wakati lile la Mbeya City lilipachikwa na Peter Mapunda.
Katika Mechi nyingine ya Ligi iliyochezwa Leo huko Kambarage, Stand United waliitungua Simba Bao 1-0.
Mechi ya mwisho hii Leo itachezwa Usiku huu huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kati ya Azam FC na Tanzania Prisons.

No comments:

Rais Dkt. Samia Awasili Addis Ababa Kushiriki Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi wa AU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bole, Jij...