Monday, February 23, 2015

YANGA YAICHAPA MBEYA CITY 3-1

MRISHO-NGASSA

VINARA wa Ligi Kuu Vodacom, Yanga, jana huko Sokoine, Jijini Mbeya wamepaa kileleni wakiwa Pointi 5 mbele ya Timu ya Pili na Mabingwa Watetezi, Azam FC, baada ya kuichapa Mbeya City Bao 3-1.
Bao za Yanga hii Leo zilifungwa na Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Amisi Tambwe wakati lile la Mbeya City lilipachikwa na Peter Mapunda.
Katika Mechi nyingine ya Ligi iliyochezwa Leo huko Kambarage, Stand United waliitungua Simba Bao 1-0.
Mechi ya mwisho hii Leo itachezwa Usiku huu huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kati ya Azam FC na Tanzania Prisons.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...