Thursday, February 19, 2015

WAZIRI CHIKAWE ATUA NCHINI MAREKANI KUSHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUPAMBANA NA VURUGU NA UGAIDI DUNIANI

mula1 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akikaribishwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula wakati Waziri huyo alipowasili ubalozini hapo jijini Washington DC kujiandaa kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani unaotarajiwa kufanyika jijini humo kesho. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
mula2 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (katikati) akimsalimia Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, jijini New York, nchini Marekani, Tuvako Manongi wakati Waziri huyo alipowasili ubalozi wa Tanzania nchini humo uliopo katika Jiji la Washington DC kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani unaotarajiwa kufanyika jijini humo kesho. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
mula3 
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula (katikati) akimtambulisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (watatu kulia) Maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo wakati Waziri huyo alipowasili ofisini hapo, jijini Washington DC kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani unaotarajiwa kufanyika jijini humo kesho. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
mula4 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wanne kulia) akizungumza na Maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani baada ya Waziri huyo kuwasili ubalozini hapo jijini Washington DC kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani unaotarajiwa kufanyika jijini humo kesho. Katikati ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
mula5 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (katikati), Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula (kushoto) na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, jijini New York, nchini humo, Tuvako Manongi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumpokea Waziri huyo aliyewasili jijini Washington DC kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani unaotarajiwa kufanyika jijini humo kesho. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments: