Friday, February 20, 2015

SAFARI YA MWISHO YA DCP MSTAAFU WA JESHI LA POLISI TANZANIA , MZEE ANDREW MICHAEL KUMALILWA HUKO TABATA SEGEREA.

 Jeneza lenye Mwili wa marehemu Mzee Andrew Michael Kumalilwa ukiwa tayari kushushwa nyumbani kwake Tabata Segerea ambapo misa ya kumuombea na kutoa heshima za mwisho zilifanyika kabla ya Kwenda kuupumzisha Mwili wake katika Nyumba yake ya Milele.
Askari wa Jeshi la Polisi Tanzania wakiwa wamebeba jeneza lenye Mwili wa aliyekuwa DCP Mstaafu wa Jeshi la Polisi Tanzania Mzee Andrew Michael Kumalilwa  wakiingia katika nyumba yake iliyopo Tabata Segerea kwaajili ya Misa na ndugu, jamaa na marafiki kutoa heshima za mwisho kabla ya kwenda kuupumzisha katika Nyumba yake ya Milele ambapo Marehemu alizikwa katika nyumba kwake Tabata Segerea.
 Mtoto wa Kwanza wa Marehemu Andrew Michael Kumalilwa, Patricia Andrew akiwa mwenye huzuni wakati wa msiba wa marehemu Baba yake ambapo marehemu alikuwa mstaafu wa jeshi la Polisi Tanzania akiwa na Cheo cha DCP.
 Jeneza lililokuwa limebeba Mwili wa Marehemu Mzee Andrew Michael Kumalilwa ukitolewa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwaajili ya kuelekea nyumbani Kwake Segerea ambapo mazishi yalifanyika
 Baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi Tanzania wakitoa heshima mbele ya jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mzee Andrew Michael Kumalilwa ambae alikuwa mstaafu wa jeshi la Polisi kwa ngazi ya DCP
 Ndugu wa marehemu akijadiliana jambo na Mmoja wa Askari wa Jeshi la Polisi wakati wa Kutoa Heshima za mwisho kabla ya kwenda kuupumzisha mwili wa Mzee Andrew Kumalilwa ambae alizikwa nyumbani kwake Tabata Segerea tarehe 14 Februari 2015.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi Tanzania, DCP Simon Siro akitoa maneno mafupi kabla ya kwenda kuupumzisha Mwili wa marehemu Mzee Andrew Kumalilwa katika nyumba yake ya Milele. Marehemu Andrew Kumalilwa alizikwa mnamo tarehe 14 February 2015 huko Nyumbani Kwake Tabata Segerea.

No comments: