Monday, March 11, 2013

Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana Watua Ethiopia Muda Huu Ukielekea Nchini China

 Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Profesa  Joram Mukama Biswalo (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kushoto), baada ya kumpokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Ndege wa Kimataifa wa Adis Ababa, akitua kwa muda kwenye Uwanja huo akiwa safarini kwenda China kwa ziara ya kikazi. Wengine kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu na Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu, Titus Kamani.
 Msaidizi wa Katibu Mkuu wa CCM, Edward Mpogolo (kushoto) na Ofisa anayeshughulikia Siasa za Kimataifa, Makao Makuu ya CCM, Amos Siantemi wakiratibu taratibu za safari ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kwenda China, leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Maofisa hao pia walikuwa sehemu ya msafara huo.
 Mkuu wa Kitengo cha Itifaki na Uhusiano wa Kimataifa wa Makao Makuu ya CCM, D. U. H. Mshana na Mkuu wa Kitengo cha Sera za Jamii na Mahusiano ya Umma, Jasinta Mboneko  na Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ya CCM, Juliana Chitinka wauaga ujumbe wa CCM wakati ukiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliokuwa ukienda china kwenye ziara ya kikazi ya siku kumi ikiongozwa na Kinana.
 Baadhi ya viongozi na maofisa wa Chama waliopo kwenye msafara huo wakiwa kwenye basi maalum kwenda kupanda ndege ya Ehiopian Airlines wakati wa safari hiyo,
Baadhi ya viuongozi na maofisa wa Chama wakiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Addis Ababa baada ya msafara wa Kinana kutua kwa saa sita kwa ajili ya kuendelea na safari ya kwenda China jioni hii.Picha zote na Bashir Nkoromo

No comments: