Saturday, March 16, 2013

JOTO HASIRA YA LADY JAYDEE ILIVYOZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM


Mkongwe wa Muziki wa Kizazi kipya, Judith Wambura Mbibo almaarufu, Lady Jaydee usiku wa kumkia leo alifanya uzinduzi wa video yake mpya aliyomshirikishja Mkongwe Mwezake katika burudani hiyo, Joseph Haule ‘Prof. J’ Video ya Wimbo unaokwenda kwa jina la ‘JOTO HASIRA’.
Jaydee alifanya uzinduzi huo katika mgahawa wake wa Nyumbani Longe uliopo Namanga wilayani Kinondoni Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mamia ya wapenzi wa Burudani na muziki wa mwana dada huyo.
Uzinduzi huo ulisindikizwa na bendi ya Lady Jaydee ya Machozi Band na kutoa burudani ambayo ilikonga nyoyo za mashabiki wake.
Pichani juu ni Lady Jaydee akiimba wimbo wake huo mpya wa Joto Hasira kwaheri shida, mbele ya mashabiki wake wakati wa uzinduzi wa video ya wimbo huo.



Jaydee akiwa kando ya gari lake mara baada ya kuwasili Nyumbani Lounge tayari kwaajili ya uzinduzi wa Video yake mpya ya Joto Hasira.
Lady JayDee akitoa burudani mbele ya mashabiki wake

Lady JayDee akifanyiwa mhojiano na vyombo mbalimbali vya habari zikiwepo Televisheni, magazeti, Redio na Blogs, ambazo zilituma wawakilishi wao katika uzinfduzi huo.

 Ben Paul nae alikuwepo Nyumbani Longe kushuhudia uzinduzi huo wa JOTO HASIRA hapa akishow love na washkaji
 Prof.J ameshiriki katika wimbo huo wa Lad JayDee Joto Hasira nae alikuwepo Ukumbini hapo, hapa akipiga picha na Warembo walio pamba show hiyo.
 Wadau mbalimbali walikuwepo kutoka pande mbalimbali za jiji la Dar es Salaam.
Nyumbani Longe ilijaa vilivyo watu mbalimbali kuanzia walio na majina hadi akina wewe na mimi.

No comments: