Thursday, March 14, 2013

Chuo Kikuu cha Waandishi wa habari chawapongeza washiriki miss utalii Tanzania taifa 2012/13

 Raisi wa Miss Utalii Tanzania Ndugu Erasto G. Chipungahelo akimkaribisha Mratibu wa masoko wa Chuo kikuu cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma.
Mratibu wa Masoko wa Chuo kikuu cha waandishi wa Habari Bi Sophia akiwakaribisha washiriki wa Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 Chuoni hapo.
Mratibu wa Masoko wa Chuo kikuu cha Waandishi wa Habari na Mawasiliano Bi Sophia Akizungumza Jambo na Washiriki wa Miss Utalii Tanzania 2012/13 .
 Washiriki wa Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 wakiwa wanajiandaa kusikiliza mambo kadhaa kutoka kwa Mratibu wa Masoko Bi Sophia.
Washiriki wa Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 wakiwa katika picha ya Pamoja na Mratibu wa Masoko wa Chuo Kikuu cha waandishi wa habari na Mawasiliano.
--
Chuo Kikuu cha Waandishi wa kimewapongeza Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 kwa elimu walizo nazo na kuwasihi watumie elimu zao kutangaza utalii wa Tanzania Jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa jamii ya Watanzania Akizungumza na washiriki hao Kijitonyama Jijini Dar es salaam, 

Mratibu wa masoko wa chuo hicho ndugu Sophia Ndibalema aliwataka kutumia Fulsa ya kuwa warembo hasa utalii kwa kujitaftia nafasi zaidi za elimu ya juu   kwa manufaa yao Jamii na Taifa kwa ujumla, alisema nafasi zipo wazi kwa wale wenye kuhitaji na wenye sifa za kujiunga chuoni hapo kwa nafasi ya Cheti, Diploma na Shahada, alisema amefurahishwa na muonekano wa asili na mavazi ya heshima kwa washiriki hao hivyo kuondoa dhana kuwa washiriki wa urembo kuwa ni wale wanaovaa mavazi yenye  Kudhalilisha jamii hii inathibitisha kuwa Miss Utalii ni Zaidi ya Mashindano Mengine na ni Alama ya Urithi wa Taifa na kielelezo cha mwanamke au Binti wa Kitanzania

No comments: