Wednesday, March 20, 2013

RAIS KIKWETE AHANI MSIBA WA TRAFIKI ALIYEGONGWA NA GARI AZINDUA MAABARA YA KISASA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku medali mmoja ya wauguzi wakongwe nchini aliyewahi pia kuwa Mbunge na Msajili wa Wauguzi na Wakunga Mama Jitto Ram  wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga katika bustani ya Mnazi Mmoja Jana  Machi 19, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweha saini kitabu cha maombolezo alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani aliyegongwa na gari baada ya msafara wa Rais kupita jana WP 2942 Koplo Elikiza nyumbani kwa marehemu sehemu za Ununio ,jana Machi 19, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa mkono wa pole  mume wa marehemu alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani aliyegongwa na gari baada ya msafara wa Rais kupita jana WP Koplo Elikiza nyumbani kwa marehemu sehemu za Ununio ,jana Machi 19, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwafariji mume wa marehemu na watoto pamoja na IGP Saidi Mwema alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani aliyegongwa na gari baada ya msafara wa Rais kupita jana WP Koplo Elikiza nyumbani kwa marehemu sehemu za Ununio ,jana Machi 19, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua kitabu cha historia ya Uuguzi na Ukunga nchini wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania  katika bustani ya Mnazi Mmoja jana Machi 19, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiondoka baada ya kufungua rasmi Maabadara ya kisasa ua Uhandisi Jeni (Genetic Engineering) katika kituo cha utafiti wa Kilimo cha Mikocheni jijini Dar es salaam jana Machi 19, 103. Kushoto ni Dkt Chrtistopher Chiiza na wa pili kulia ni Mku wa kituo hicho Bw. Joseph Ndunguru.Picha na IKULU

No comments: