Monday, March 04, 2013

Waziri wa Mambo ya Nje, Membe akutana kwa mazungumzo na aliyekuwa Katibu wa Baraza la Mawaziri la Japan

 Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo huku ujumbe kutoka Japan ukimsikiliza.
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akizungumza na  aliyekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Mawaziri wa Japan, Bw.Osamu Fujimura alipofika na ujumbe wake Ofisini kwa Mhe. Waziri leo ambapo walizungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japan ikiwemo maandalizi ya Mkutano wa Tano unaohusu Ushirikiano kati ya Japan na Afrika (TICAD V) utakaofanyika nchini humo mwezi Juni 2013. 
 Mhe. Membe akimsikiliza Bw. Fujimura wakati wa  mazungumzo yao.
 Mhe. Masaki Okada (kulia), Balozi wa Tanzania hapa nchini akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati ujumbe kutoka Japan ulipomtembelea Mhe. Membe ofisini kwake. Wengine katika picha ni Balozi Mbelwa Kairuki (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Khatib Makenga, Afisa katika Idara hiyo.
Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Bw. na Bibi Fujimura (kushoto) na Mhe. Masaki Okada (kulia), Balozi wa Japan hapa nchini mara baada ya mazungumzo.Picha Zote na Tagie Daisy Mwakawago-Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

No comments: