Saturday, March 16, 2013

Jeshi la Polisi Lapiga Marufuku Maandamano ya Chadema Leo, Latoa Sababu Za Kupiga Marufuku Maandamano Hayo


  Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo ACP, Charles Kenyela
---
Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kanda ya Kinondoni limekataza maandamano yaliyokuwa yamepangwa kufanyika tarehe 16 Machi 2013 yaliyokuwa yameiratibiwa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika yaliyolenga kufika katika Wizara ya Maji ili kufikisha ujumbe kwa Waziri wa Maji, Prof Maghembe kuhusu kero ya maji katika jimbo hilo ambayo haijatatuliwa wala kupatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu. Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo ACP, Charles Kenyela amesema endapo maandamano hayo yatafanyika:
   
 1. Upo wasiwasi wa kutokea kwa vurugu pale watakaposhindwa kufikia muafaka kuhusu hoja zao.
2. Amewasiliana na Ofisi ya Waziri husika na kufahamishwa kuwa haina  taarifa rasmi za ujio wa maandamano hayo.

 3. Barabara yatakakopita maandamano hayo ipo katika ujenzi na hivyo  maandamano hayo yatazuia shughuli za mkandarasi kukamilisha kazi yake kwa  wakati na kuisababishia Serikali hasara.
  4. Eeo ambamo maandamano hayo yanakusudiwa kutamatia ni dogo na hivyo  itasababisha usumbufu mkubwa

No comments: