Wednesday, June 08, 2016

SSRA YATOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KWA WAKULIMA, VYUO VYA UALIMU NA VETA KATIKA MIKOA YA RUKWA, KIGOMA NA KATAVI

Mgeni rasmi Kaimu RAS Mkoa wa Rukwa Bw. Abubakary Kunenge, akitoa hotuba wakati wa ufungizi wa semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wakulima wa MVIWATA Rukwa, Kulia ni Mwenyekiti wa MVIWATA Rukwa Bi. Lydia Ruhilo na kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Mohamed Nyasama.
Sehemu ya Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Sumbawanga wakisikiliza kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kutoka SSRA wakati wa Semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii Mkoani Rukwa hivi karibuni.
Afisa wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Samuel Nzunda akiwasilisha mada wakati wa semina ya elimu ya Hiafadhi ya Jamii mkoani Rukwa.
Wawakilishi kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi wa Chuo cha VETA-Kigoma mara baada ya semina ya elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoendeshwa na SSRA mkoani humo hivi karibuni.

No comments: