Monday, June 20, 2016

TAASISI YA UONGOZI NA CHUO CHA UTAWALA CHINA ZATIA SAINI HATI YA MAKUBALIANO

  Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (aliyeketi kulia) na Makamu wa Rais wa Chuo cha Utawala China Bw. Chen Li (aliyeketi kushoto) wakisaini hati za makubaliano ya ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili mapema leo jijini Dar es Salaam. Katika makubaliano hayo, Chuo cha Utawala China kitatoa fursa kwa watumishi wa umma nchini Tanzania kwenda kupokea mafunzo ya kiutawala nchini China, pamoja maandalizi ya makongamano tofauti tofauti na utoaji wa mihadhara kuhusu utawala, maendeleo ya majiji na ‘Kufahamu zaidi China’ yatakayofanyika hapa nchini na China. 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (kulia) na Makamu wa Rais wa Chuo cha Utawala China Bw. Chen Li (kushoto) wakibadilishana hati za makubaliano ya ushirikiano baada ya kusaini hati hizo mapema leo jijini Dar es Salaam zenye malengo ya kutoa mafunzo ya kiutawala kwa watumishi wa umma nchini.
 Ujumbe kutoka Chuo cha Utawala China na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Uongozi wakiendelea na mazungumzo wakati wa tafrija fupi ya utiaji saini ya hati za makubaliano kati ya Taasisi hizo mbili zenye malengo ya kuongeza ufanisi serikalini kupitia mafunzo kwa watumishi wa umma.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa akizungumza wakati wa tafrija fupi ya kusaini hati za makubaliano kati ya Taasisi ya Uongozi na Chuo cha Utawala China. 
 Makamu wa Rais wa Chuo cha Utawala China Bw. Chen Li akizungumza wakati wa tafrija fupi ya kusaini hati za makubaliano kati ya taasisi yake ya Chuo cha Utawala China na Taasisi ya Uongozi.

No comments: