Monday, June 27, 2016

TASAF YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA.

 Watumishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF wakiwa katika kilele cha wiki ya Utumishi wa Umma kwenye ukumbi wa Mikutano wa Taasisi hiyo jijini Dar Es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa TASAF wakiwa katika Mkutano wa kilele cha Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma uliojadili namna ya kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
 Baadhi ya wafanyakazi wa TASAF wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo Bwana Ladislaus Mwamanga, ( hayupo pichani) kujadili uboreshaji wa huduma za mfuko huo katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bwana Ladislaus Mwamanga ( aliyeshika kipaza sauti) akitoa ufafanuzi juu ya moja ya masuala yaliyoulizwa na wafanyakazi (hawapo pichani) katika kikao cha kufunga wiki ya utumishi wa umma yaliyofanyika katika ofisi za makao makuu ya taasisi hiyo jijini Dar esa salaam.
Na Estom Sanga-TASAF.
WAFANYAKAZI wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF wameadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa Menejimenti ya taasisi hiyo kukutana nao kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam na kusikiliza kero zao kwa lengo la kuzitafutia ufumbuzi ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Mfuko huo wa Maendeleo ya Jamii unaotekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini , unatoa huduma kwa Zaidi ya Kaya Milioni Moja na Lakini Moja nchini kote jukumu iliyopewa na serikali katika jitihada zake za kupambana na Umaskini nchini..

Imearifiwa katika kikao hicho kuwa mafanikio makubwa yameanza kujitokeza kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambapo wengi wao wameanza kujiwekea misingi ya kupunguza umaskini kwa kuwa na uwezo wa kusomesha watoto,kupata huduma za afya,kuwa na uhakika wa lishe na kuongeza uchumi wao.

No comments: