Tuesday, March 11, 2014

Kamati Kuu Chadema, yampitisha Mathayo Torongey kuwa mgombea rasmi wa ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze

Mgombea Ubunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chadema, Mathayo Torongey akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana baada ya kutambulishwa. Picha na Michael Jamson  
----
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimempitisha Mathayo Torongey kuwa mgombea rasmi wa ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze.

Akimtambulisha mgombea huyo kwa Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa Chadema, John Mrema alisema Torongey alipitishwa juzi na Sekretariati ya chama kwa niaba ya kamati kuu.
“Kikao cha Sekretariati kilizingatia maoni na ushauri wa wanachama na viongozi wetu wa ngazi za chini, Hivyo kwa kuwa hakukuwa na kipingamizi chochote juu ya agombea, chama kilimpitisha Torongey” alisema Mrema.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.....

No comments: