Monday, March 17, 2014

KALENGA WAPIGA KURA ULIVYOKUWA

 Wakazi wa Kalenga A wakiwa kwenye wamejipanga mstari wakati wa kupiga kura ambapo vyama vitatu vimesimamisha waogombea katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga vyama hivyo ni CCM,CHAUSTA na CHADEMA.
Wakina Mama wa Kalenga A wakiangalia majina yao kwenye orodha ya wapigaji kura iliyobandikwa kwenye kituo cha upigaji kura.
Bibi Zaina Konji akipata msaada kutoka kwa Susan Madugulu wakati wa upigaji kura kata ya Ulanda kijiji cha Mangalali.
 Bibi Zaina Konji akipiga kura kutimiza haki yake ya kisheria katika kumchagua mbunge wake wa jimbo la Kalenga atakayewaongoza katika kipindi kilichobaki.
 Msimamizi wa kituo cha kupiga kura kata ya Ulanda Lenny Kikungwe akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliojitokeza kupiga kura .
 Uhakiki wa jina la mpiga kura ukifanywa kwa umakini wakati zoezi la upigaji kura likiendelea katika uchaguzi mdogo wa Kalenga. Picha zote za Fullshangwe

No comments: