Tuesday, March 11, 2014

Mgombea wa Ubunge jimbo la Kalenga kupitia tiketi ya CCM Ndugu Godfrey Mgimwa Aendelea na Kampeni Kitongoji cha Tosamaganga na Kalenga


Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu akihutubia wakazi wa kitongoji cha Tosamaganga wakati wa kampeni za kumnadi mgombea wa Ubunge jimbo la Kalenga kupitia tiketi ya CCM Ndugu Godfrey Mgimwa ambapo aliwaambia wananchi hao tutafute viongozi wa mfano wa Kitanzania ambao hawatatuchonganisha na watoto wao.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu akipokea kadi ya Chadema iliyorudishwa na Ndugu Said Omary Mbilinyi ambaye amerudi CCM baada ya kutoelewa sera na siasa za Chadema.
Diwani wa kata ya Kalenga Ndugu Maria Galinoma akihutubia wakazi wa kitongoji cha Tosamaganga wakati wa kumnadi mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM Ndugu Godfrey Mgimwa.
Msanii maarufu Tanzania mwenye vipaji vya kuigiza ,kucheza na kuimba Dokii akiimba na kucheza pamoja na Diwani wa Viti Maalum na Mwenyekiti wa UWT Iringa Vijijini Ndugu Shakira Kiwanga wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge za CCM kwenye kitongoji cha Tosamaganga.
Chifu Abdul Adam Sapi Mkwawa akiwahtubia wakazi wa Kalenga A,wakati wa mkutano wa kampeni za Ubunge kupitia CCM na kusema yeye mpaka kufa kwake ni CCM na kamwe asitafsiriwe vinginevyo.
Mtela Mwampamba akihutubia wakazi wa kitongoji cha Tosamaganga na kuwaambia wana Kalenga wasikubali kutumika kama wajinga waliwao kwani Chadema haijui mahusiano kati ya hospitali,barabara,huduma za jamii na serikali ya Chama Cha Mapinduzi.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mtwara Ndugu Shaibu Akwilombe akihutubia wakazi wa kijiji cha Tosamaganga wakati wa kumnadi mgombea wa kiti cha ubunge kupitia CCM Ndugu Godfrey Mgimwa.
Sister Paula Msambwa mwenye umri wa miaka 73 na aliyewahi kuwa mwalimu wa Marehemu William Mgimwa kuanzia darasa la kwanza mpaka la nne ambapo alimfundisha somo la hisabati amesema amefarijika kumuona mtoto wa mwanafunzi wake akigombea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Kalenga.Picha na Adam Mzee

No comments: