Pichani
 kulia ni Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga akiwakaribisha 
wageni wake, akiwemo mwanamuziki nyota wa dansi ndani ya kundi la Wenge 
BCBG,kutoka nchini DRC-Congo, JB Mpiana (pichani kati) kwenye hafla fupi 
ya chakula cha usiku iliyofanyika kwenye kiota cha maraha cha Escape 
2, kilichopo Kunduchi jijini Dar, hafla hiyo pia ni sehemu ya muendelezo 
wa shamra shamra za maadhimisho ya miaka 13 ya Clouds FM tangu 
kuanzishwa kwake hapa nchini.

 Mkurugenzi
 wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga akiwakaribisha wageni wake na 
kuzungumza nao machache na kuhakikisha wanapatiwa chochote kitu.

 Mkurugenzi
 wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimtambulisha mke wake Johayna 
Kusaga  (ambaye ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Prime Time 
Promotions Ltd) kwa Mwanamuzik JB Mpiana na kwa wageni wengine waliofika
 kwenye hafla hiyo ya chakula cha pamoja.

 Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimkaribisha mgeni wake JB Mpiana kwenye chakula

 Pichani
 ni baadhi ya Washiriki wa shindano la Miss East Afrika  2012 ambao pia 
walialikwa kwenye chakula cha pamoja ndani ya kiota cha maraha cha 
Escape 2,kilichopo Kunduchi jijini dar.

 Washiriki wa shindano la Miss East Afrika wakiwa katika picha ya pamoja

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Cassim akitumbuiza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali 

 Boniventure
 Kilosa a.k.a Dj Venture alikamata mashine na kuangusha ngoma kali 
zikiwemo za Kinaija,abazo wageni wengi walionekana kuburudishwa nazo 
vilivyo.

 Washiriki wa shindano la Miss East Afrika 2012 wakijiachia vilivyo kwa mikato ya ngoma iliokuwa ikiangushwa na Dj Venture.

 Joseph
 Kusaga a.k.a Boss JOe akizungumza na baadhi ya wasanii mahiri wa muziki
 wa kizazi kipya,Ay na Mwana FA ndani ya hafla fupi ya chakula cha usiku
 kulichoandaliwa kwa ajili ya wageni.

 Wadau nao walikuwepo.Mdau wa MJ FM pamoja na Andrew Kusaga wakishoo love.
|  | 
| Wafanyakazi mbalimbali kutoka Clouds Media Group walikuwepo pia | 

Kuserebuka kama hivi pia kulikuwepo  .

 Mtangazaji wa Clouds TV,Ben Kinyaiya akifanya mahojiano mafupi na mwanamuziki mkongwe wa dansi,Ndandaa Kossovo.

 Dj Venture na mshkaji wake wakivuta pumzi.

 Mmoja
 wa Wakurugenzi wa Prime Time promotios,pichani kulia Godfrey Kusaga 
akibadilishana mawazo na Mtangazaji mahiri wa kipindi cha Jahazi cha 
Clouds FM,Ephrahim Kibonde huku wakiangusha moja moja.

 Mazungumzo ya hapa na pale pia yalikuwepo.

Pichani shoto ni Dj Bon Love,Balozi,Godliva pamoja na Ephraim Kibonde wakishoo love.

 
 
No comments:
Post a Comment