
 
 Meneja Mkuu wa kiwanda cha TANPACK TISSUES Ltd. Bw. Rajesh Shah 
akimuonyesha Mh. Naibu Waziri Charles Kitwanga sehemu maalum ya kuchujia
 maji taka yanayotoka katika kiwanda hicho.

 Meneja
 Mkazi wa Kampuni ya BIDCO inayotengeneza mafuta ya kula na sabuni Bw. 
Hemal Shah akimuogoza Mh. Kitwanga kukagua tenki linalohifadhi uchafu 
baada ya kutengeneza sabuni ambao pia husafishwa kitaalamu kupunguza 
kemikali zilizomo ndani yake.

 
Pichani Juu na Chini Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais
 (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akikagua matenki hayo wakati wa ziara 
hiyo aliyoambatana na wanahabari pamoja na viongozi wa NEMC.


 
Maafisa wa Wizara, NEMC na baadhi ya wanahabari wakiangalia taratibu 
zinazopitiwa kupitisha na hatimaye kusafisha maji taka ya viwanda kabla 
ya kwenda kuyamwaga katika maeneo ya wazi.

Naibu Waziri Mh. Kitwanga akitoa agizo kwa Uongozi wa BIDCO wakati wa ziara ya kukagua viwanda mbalimbali jijini Dar es Salaam.

 Naibu
 Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles 
Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhitimisha awamu 
ya kwanza ya ziara ya kutembelea viwanda vya jijini Dar es Salaam ambapo
 amesema ziara hiyo imempa nafasi ya kujionea hali halisa ya viwanda vya
 jijini na kugundua kuwa vingi havina mitambo ya kusafisha maji machafu 
yanayokwenda kumwagwa kwenye mito na kushuhudia kuwa vingine havina 
viwango vya kupeleka maji taka yake kwenye mtandao wa maji taka ya 
DAWASCO na kuwataka kufikia viwango vinayokubalika na mazingira yetu.

Msafara
 wa Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh. 
Charles Kitwanga ukiondoka mara baada ya kumaliza ngwe ya kwanza ziara 
ya Kukagua Viwanda kuangalia hali halisi jinsi viwanda hivyo vinafuata 
kanuni za utunzaji mazingira. PICHA ZA FULL SHANGWE
 
 
No comments:
Post a Comment