Thursday, December 06, 2012

WAZIRI KITWANGA AFANYA ZIARA YA GHAFLA VIWANDANI JIJINI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA SHERIA


Meneja Mkuu wa kiwanda cha TANPACK TISSUES Ltd. Bw. Rajesh Shah akimuonyesha Mh. Naibu Waziri Charles Kitwanga sehemu maalum ya kuchujia maji taka yanayotoka katika kiwanda hicho.

Meneja Mkazi wa Kampuni ya BIDCO inayotengeneza mafuta ya kula na sabuni Bw. Hemal Shah akimuogoza Mh. Kitwanga kukagua tenki linalohifadhi uchafu baada ya kutengeneza sabuni ambao pia husafishwa kitaalamu kupunguza kemikali zilizomo ndani yake.

Pichani Juu na Chini Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akikagua matenki hayo wakati wa ziara hiyo aliyoambatana na wanahabari pamoja na viongozi wa NEMC.


Maafisa wa Wizara, NEMC na baadhi ya wanahabari wakiangalia taratibu zinazopitiwa kupitisha na hatimaye kusafisha maji taka ya viwanda kabla ya kwenda kuyamwaga katika maeneo ya wazi.

Naibu Waziri Mh. Kitwanga akitoa agizo kwa Uongozi wa BIDCO wakati wa ziara ya kukagua viwanda mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhitimisha awamu ya kwanza ya ziara ya kutembelea viwanda vya jijini Dar es Salaam ambapo amesema ziara hiyo imempa nafasi ya kujionea hali halisa ya viwanda vya jijini na kugundua kuwa vingi havina mitambo ya kusafisha maji machafu yanayokwenda kumwagwa kwenye mito na kushuhudia kuwa vingine havina viwango vya kupeleka maji taka yake kwenye mtandao wa maji taka ya DAWASCO na kuwataka kufikia viwango vinayokubalika na mazingira yetu.

Msafara wa Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh. Charles Kitwanga ukiondoka mara baada ya kumaliza ngwe ya kwanza ziara ya Kukagua Viwanda kuangalia hali halisi jinsi viwanda hivyo vinafuata kanuni za utunzaji mazingira. PICHA ZA FULL SHANGWE

No comments: