Louise Kamin Meneja Mradi wa 
Media For Development International Tanzania akizungmza kuelezea filamu 
ya Siri ya Mtungi ilyotengenezwa na taasisi hiyo itakayokuwa ilirushwa 
na vituo vya televisheni vya ITV na EATV ikiwa na maudhui ya maisa  
katika familia ya jamii  inayohamasishwa  na  penzi, 
 lililoletwa  na  woga,  ushirikina  na  usaliti,  ikinyanyuliwa  na 
 ucheshi  na  furaha,  na  kupewa  nguvu  ya  mshikamano  wa  ndani  wa 
 familia  na  urafiki. Uzinduzi wa filamu hiyo ulifanyika jana kwenye 
ofisi za shirika hilo Msasani jijini Dar es salaam
Baadhi ya waandishi wa habari na
 wageni walioalikwa katika uzinduzi huo uliofanyika katika ofisi za 
shirika hilo Msasani jijini Dar es salaam.
Baadhi ya washiriki waliocheza katika filamu hiyo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo jana.
………………………………
Tamthilia  mpya  kabisa  ya  Televisheni  kutoka  kwa  Watu  wa  Marekani!  Onyesho  la  Kwanza  la  SIRI  YA  MTUNGI  litakuwa  
ITV  saa  3.30  usiku  tarehe  9  Desemba.  Na  EATV  saa  3.30  usiku  tarehe  12  Desemba.
Mchanganyiko  mzuri  wa  wahusika  wa  Siri  ya  Mtungi,  waliohusiana  kwa  damu  au  ndoa,  au  kwa  mapenzi  tu,  unaunda  
jamii  inayohamasishwa  na 
 penzi,  lililoletwa  na  woga,  ushirikina  na  usaliti,  ikinyanyuliwa
  na  ucheshi  na  furaha,  na  
kupewa  nguvu  ya  mshikamano  wa  ndani  wa  familia  na  urafiki.    
Tamthilia  hii  ya  Televisheni 
 ni  Programu  ya    awali  ya  TCCP  (Tanzania  Communications 
 Capacity  Project)  iliyotekelezwa  
na  JHU-‐CCP  (Johns  Hopkins  Bloomberg  School  of  Public  Health  Center  for  Communications  Programs)  kwa  msaada  
wa  USAID  (United  States  Agency  for  International  Development)  na  kama  sehemu  ya  PEPFAR  (US  President’s  
Emergency  Fund  for  AIDS  Relief).  
Ikiwa  imetayarishwa  na  MFDI  (Media  For  Development  International),  Siri  ya  Mtungi  inawaleta  pamoja  Wasanii  bora  
wa  Tanzania,  waandishi,  wana  mitindo  ya  nguo,  wakurugenzi  wa  sanaa,  waigizaji  na  watendaji  wa  filamu  kwenye  
mafanikio  makubwa  ya  ukuaji  wa  tasnia  ya  filamu  na  televisheni  Tanzania.    
Kati  ya  mitaa  yenye  harakati
  nyingi  ya  Dar  es  Salaam  na  ile  iliyo  kimya  ya  Bagamoyo, 
 tunapenya  nyuma  ya  milango  
iliyofungwa  mpaka  kwenye  maisha  ya  Cheche  na  mkewe  Cheusi,  binti  wa  kiongozi  maarufu  katika  jamii,  mwenye  
wake  wengi,  Mzee  Kizito, 
 pamoja  na  wahusika  wengine  kama  Duma,  mwana  DJ;    Lulu-‐ 
 shangingi  lililokubuhu;  Farida-‐  
roho  ya  nyoka;  Masharubu-‐  mzee  kikwekwe  na  wengine  wengi.        
RATIBA  YA  ITV:   Jumapili  3.30  usiku        -‐          Jumatano  3.30  usiku  
RATIBA  YA  EATV:  Jumatano  10.30  Alasiri        -‐          Alhamisi  7.00  Mchana        -‐          Jumamosi  10.30  Alasiri



 
 
No comments:
Post a Comment