Wednesday, December 05, 2012

WAKAZI WA BUNJU, WAZO WAFURAHIA WAZIRI PROFESA TIBAIJUKA KUVALIA NJUGA MGOGORO WAO NA KIWANDA CHA SARUJI WAZO HILL

 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka akiwasalimia wakazi wa kata ya Bunju na Wazo mara baada ya kuwasili katika eneo  hilo  kwa lengo la kuzungumza nao ili kutafuta suluhisho la kudumu la  mgogoro wa ardhi kati yao na  kiwanda cha Saruji cha Twiga jana jioni.
(PICHA NA ARON MSIGWA WA MAELEZO)
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka akiongea katika mkutano wa hadhara na maelfu ya wakazi wa kata ya Wazo na Bunju waliojitokeza kufuatilia maendeleo ya mgogoro wa ardhi kati yao na Kiwanda cha Twiga Cement ambapo pamoja na mambo mengine amewahakikishia wakazi hao kuwa mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kuwaomba kutoa ushirikiano kwake.
 
Diwani wa eneo la Bunju na Wazo Sharif Exavery Majisafi akiongea na wananchi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka kuzungumza nao.
 
Sehemu ya umati mkubwa wa wakazi wa kata za Bunju na Wazo wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka.
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka akipitia baadhi ya nakala za ramani zinazoonyesha eneo la Kata ya Bunju na Wazo pamoja na Kiwanda cha Saruji cha Twiga ambazo ziligawiwa kwa wananchi. Kushoto ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Silasi Mayunga
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akiongea na Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha Saruji cha Twiga (Twiga Cement) Bw.Pascal Lessoinne (kushoto) mara baada ya mkurugenzi huyo kutoa taarifa fupi ya maendeleo ya kiwanda hicho na hali ya mvutano wa muda mrefu wa umiliki wa maeneo baina ya wakazi wa kata za Bunju na Wazo jijini Dar es salaam.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja  katikati ya wananchi wenzake akiwa amevaa kofia ngumu ya waendesha pikipiki wakati wa mkutano wa hadhara wa wakazi wa kata ya Bunju na Wazo na Waziri wa Ardhi Prof. Anna Tibaijuka kujadili mgogoro wa ardhi kati yao na Kiwanda cha Twiga Cement. Haikujulikana mara moja lengo la kuvaa kofia hiyo licha ya mkutano huo kutawaliwa na amani na maelewano makubwa.

No comments: