Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila 'RAY C' 
akimshukuru Rais Kikwete kwa msaada wa matibabu aliompatia ikulu jijini 
Dar es Salaam leo
Rais 
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Ray C (wa tatu kushoto), Mama 
yake mzazi Ray C Bibi Margareth Mtweve (kushoto) na Sarah Mtweve Dada 
yake Ray C.Picha na Freddy Maro-IKULU-
--
Na Freddy Maro, Ikulu
Mwanamuziki wa
 Kizazi Kipya Rehema Chalamila maarufu kama RAY C leo amemtembelea Rais 
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dare s Salaam na kumshukuru kwa 
msaada wa matibabu wakati alipokuwa mgonjwa hivi karibuni.
Rehema 
aliyefuatana na Mama yake Mzazi Margareth Mtweve na Dada yake Sarah 
Mtweve alimweleza Rais kuwa afya yake imeimarika na kwamba muda si mrefu
 atarejea jukwaani kukonga nyoyo za mashabiki wake.
Kwa apande 
wake, Mama Mzazi wa Ray C amemshukuru Rais Kikwete kwa kuokoa maisha ya 
mwanaye na vilevile ametoa wito kwa watu wanaokusanya michango kwa ajili
 ya mwanaye waache kufanya hivyo kwani matibabu ya Ray  C yamegharamiwa 
na Rais.
 
 
No comments:
Post a Comment