Monday, December 17, 2012

KOFII OLOMIDE ASHUSHA BURUDANI NZITO UWANJA WA CCM KIRUMBA

 
Mambo makubwa yamefanyika katika uwanja wa CCM Kirumba usiku huu  jijini Mwanza ambapo Kofii Olomide mwanamuziki Gwiji Barani Afrika kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amepagawisha mashabiki wa  wake katika tamasha la Tusker Carnival  na kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki  jijini humo, Mwanamuziki Kofii Olomide akiwa na kundi lake pamoja na mwimbaji wake Cindy amefanya kilichokuwa kikitarajiwa pamoja na hamu ya mashabiki kupiga kelele kwa madai ya kutaka kumuona mwanamuziki huyo mkali na anayekubalika barani Afrika na Ulaya.
Mwanamuziki huyo  amefanya mambo makubwa kama  burudani aliyoshusha jana kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam,  Watu mbalimbali wamejitokeza kwenye uwanja wa CCM Kirumba ili kumuona mwanamuziki huyo pichani juu akiwa na mwimbaji wake Cindy akimtambulisha kwa mashabiki wa jijini Mwanza .
Kamanda wa Fullshangblog alikuwepo   jijini Mwanza ili kukumuvuzishia moja kwa moja matukio hayo usiku huu kutoka katika uwanja wa CCM Kirumba Kaa mkao wa kuperuzi mara kwa mara katika ukurasa wa Fullshangwelog ili kujua kinachojiri uwanjani hapo .
 
Kofii Olomide na Mwimbaji Cindy wakiimba huku wakiwa amezungukwa na wanenguaji wake
 
Mwanamuziki Kofii Olomide akipanda jukwaani huku akisinddikizwa na waimbaji wake.
 
Cindy katikati Mwimbaji mahili wa kike wa mwanamuziki Kofii Olomide akiimba jukwaani kalba ya Kofii Olomide mwenyewe kupanda jukwaani.
 
Kazi iko hapa kama wanavyoonekana wanenguaji hao wakicheza kwa sataili ya aina yake.
 
Hii ilichezwa kwa kwenda mbele na kurudi nyuma huku wakiwa wameshikana.
 
Palikuwa hapatoshi kwa shoo kabambe kabisa kutoka kwa wanenguaji wa Kofii Olomide.
 
Ili mradi burudani iliyopangika kutoka kwa wanenguaji hao
 
Staili hiyo ilichezwa kwa hisia pia
 
Kutoka kulia ni Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa  (SBL), Anitha Msangi Maurice Njowoka na Patrick Kisaka kutoka kampuni ya bia ya Serengeti wakishoo love kwa picha.
 
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti Ephraim Mafuru kulia na Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga wakiwa katika picha ya pamoja
 
Wadau kutoka Miss Tanzania wakiwa katika onesho hilo.
 
Rachel wa THT akicheza na mmoja wa wanenguaji wa mwanamuziki Kofii Olomide.
 
Kofii Olomide akimpongeza msanii Rachel wa THT baada ya kuonyesha uwezo wake katika kuimba kwenye onesho hilo.
 
Waimbaji wa mwanamuziki Kofii Olomide wakiimba kwa hisia katika enesho hilo.
 
Rapa wa mwanamuziki Kofii Olomide anayejulikana kwa jina la Computar akighani huku wanenguaji wa kiume wakiingia jukwaani.
 
Jukwaani ni Recho wa kundi la  THT kutoka jijini Dar es salaam akinendelea kutoa burudani jukwaani
 
H. Baba akifanya vitu vyake mbele ya mashabiki wa jijini Mwanza wakati akitoa burudani ya utangulizi kabla ya mwanamuziki Kofii Olomide Kupanda jukwaani.
 
Pepe Kale wa Mwanza naye akafanya mambo makubwa na kukubalika na umati wa mashabiki waliohudhuria katika onesho hilo. Kwa taarifa zaidi hebu cheki FULLSHANGWE.

No comments: