Sunday, February 28, 2010

Nassib arudi tena TFF


Nchimbi (Kushoto) na Nassib (kulia) wakisubiri matokeo.
NI kawaida kuwa baada ya ushindi kuna mashamsham, lakini tofauti na jana, uchaguzi wa Makamu wa pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, ulikuwa na utulivu wa aina yake hata baada ya matokeo kutangazwa.

Mbali na wajumbe zaidi ya 100 kuchagua mgombea wa nafasi hiyo, pia walimchagua mwakilishi wa Kanda Nyanda za Juu Kusini ambaye ndiye mwakilishi katika mkutano wa TFF.

Katika nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais, John Nchimbi alikuwa akichuana na Nassib Ramadhani aliyekuwa anatetea nafasi yake.

Nassib aliyekuwa akidhaminiwa na Mtibwa Sugar huku Nchimbi akisimamiwa na Majimaji, alitetea kiti chake baada ya kupata upinzani mkali wa kura 54 wakati Nchimbi alipata 47.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na upinzani mkali huku wagombea wakiwa wamesindikizwa na wapambe wao jumla ya wajumbe 101 walipiga kura na hakuna kura hata moja iliyoaharibika.

Hata hivyo, kulikuwa na hisia za rushwa kitendo kilichowafanya baadhi ya wapambe wa wagombea kuimarisha ulinzi eneo la chooni huku wengine wakionekana kukaa vikundi vikundi. SOURCE: MWANANCHI BY VICKY KIMARO.

1 comment:

Anonymous said...

In contrast, the non-organic gardener is more likely to use chemically
created fertilizers. When you're preparing your planting area, just mix the soil with about three inches of organic compost. Each has his own concoction of soapy water, tobacco juice or hot pepper solutions to to deter these nasty pests and try those first.

Here is my weblog; coptic