Source TBC.
Mpaka sasa mkutano haujaisha ila Taarifa toka Dodoma, ni kuwa wajumbe karibu wengi kwenye mkutano wa NEC ya CCM wanapendekeza kamati ya Mzee Mwinyi iongezwe muda ili kuweza kuendelea kumalizia tofauti zilizopo baina ya wana CCM.
Katibu mwenezi wa CCM, kutoa taarifa rasmi mara tu baada ya mkutano kumalizika hata iwe saa nane ucku, atakuwa na press confrence muda huwo!!!!!!!
Lakini suala bajeti ya uchaguzi ndani ya CCM na mvutano baina ya makundi ndani ya chama ni miongoni mwa mambo yaliyozua mvutano katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (Nec) uliyomalizika jana na kushindwa kufikia hitimisho na badala yake inadaiwa kuwa walilishana yamini ili mambo yaishe.
Mazingira hayo pia yaliwafanya wajumbe wa mkutano huo kuitaka Kamati ya Mzee Ali Hassan Mwinyi iliyopewa jukumu la kuchunguza kiini cha mparaganyiko ndani ya chama hicho tawala, hivyo kuiongezea muda ili kuweka sawa baadhi ya mambo ambayo hayakuwa na majibu ya kujitosheleza.
Suala la maridhiano ya Zanzibar pia linadaiwa kuwasha moto katika mkutano huo ikidaiwa kwamba, kulikuwa na mvutano mkali miongoni mwa wajumbe, huku baadhi wakitaka tarehe ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar isogezwe mbele na wengine wakipinga.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TANZANIA YAUNGA MKONO MABADILIKO YA MFUMO WA AFYA DUNIANI
Na Hassan Kimweri, WAF - Addis Ababa Tanzania imeunga mkono juhudi za kuimarisha Shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia maboresho ya Muundo w...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...
No comments:
Post a Comment